Habari za Punde

Puma Energy Tanzania Yafutarisha Viongozi na Wadau Zanzibar

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Puma Energy Bi. Fatma Abdallah akizungumza wakati wa hafla ya Iftaar ya pamoja iliyoandaliwa na Kampuni hiyo, amesema lengo la Iftaar hiyo ni kuimarisha umoja kwani ushirikiano walionao umesaidia sana kufanikisha biashara zao hapa Zanzibar.

Kampuni ya PUMA Energy imeandaa futari maalum Zanzibar, ikikusanya pamoja wateja wake, viongozi wa dini na serikali , na wadau wakuu kwa jioni ya shukrani, mshikamano, na tafakari katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Puma Energy Bi. Fatma Abdallah amesema lengo la futari hiyo ni kuimarisha umoja kwani ushirikiano walionao umesaidia sana kufanikisha biashara zao hapa Zanzibar.

Aidha, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ina matarajio makubwa ya kutanua huduma muhimu zitakazowafikia wananchi kupitia miradi ya uwekezaji inayoanzishwa hapo nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Seif Abdallah Juma amesema lengo la kuwepo miradi hiyo ni kukuza sekta ya huduma na biashara ili kukuza pato la nchi

Kampuni ya Puma Energy Tanzania ni wauzaji wa aina mbali mbali za mafuta ya vyombo vya moto na vilainishi; Imekuwepo Zanzibar tangu mwaka 1994 (wakati huo ikijulikana kama BP Tanzania)

Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Ndg.Seif Abdallah Juma akijumuika na Wafanyakazi na waalikwa katika hafla ya Iftaar ya pamoja iliyoandaliwa na Kampinu ya Pima Energy Tanzania iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanza wa Ndege Zanzibar na (kulia kwake)Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Puma Energy Tanzania Bi. Fatma Abdallah.

Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Ndg.Seif Abdallah Juma akijumuika na Wafanyakazi na wageni waalikwa katika hafla ya Iftaar ya pamoja iliyoandaliwa na Kampinu ya Pima Energy Tanzania iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanza wa Ndege Zanzibar.


Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Seif Abdallah Juma akizungumza na kutowa shukrani kwa Uongozi wa Kampuni ya Puma Energy, wakati wa hafla Iftaar ya pamoja iliyoandaliwa na Kampuni hiyo katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Seif Abdallah Juma akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa shukrani Kampuni ya Puma EnergyTanzania,baada ya kumalizika kwa hafla Iftaar ya pamoja iliyoandaliwa na Kampuni hiyo katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.