Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi Aongoza Waumini wa Dini ya Kiislamu Katika Sala ya Eid Al Al Fitry Iyofanyika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Zanzibar

WAUMINI wa Dini ya Kiislamu  Zanzibar wakiwa katika viwanja vya Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini  Jijini Zanzibar, wakifuatilia hatuba ya Sala ya Eid Al Fitry, iliyofanyika leo 31-3-2025, baada ya kumalizika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Viongozi wa Serikali,Viongozi wa Dini na Wananchi, wakifuatilia hutuba ya Sala ya Eid Al Fitry, ikisomwa na Sheikh Khamis Gharib Khamis, baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Jijini Zanzibar iliyofanyika leo 31-3-2025 na (Kushoto kwa Rais) Mifti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kaab na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali na (kulia kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Alhajj Dkt. Haroun Ali Suleiman na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhajj Othman Masoud Othman. 











RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika kuitikia dua ikisomwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Hassan Othman Ngwali, baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid Al Fitry, iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar leo 31-3-2025 baada ya kumalizika kwa Mwezi Mtukifu wa Ramadhani, na (kushoto kwa Rais) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kaab  na (kulia kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Alhajj Dkt. Haroun Ali Suleiman na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhajj Othman Masoud Othman
BAADHI ya Viongozi wa Dini wakijumuika katika kuitikia dua ikisomwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Hassan Othman Ngwali, baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid Al Fitry, iliyofanyika katika  Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Jijini Zanzibar leo 31-3-2025




RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Saleh Omar Kaab, baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid Al Fitry iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Jijini Zanzibar leo 31-3-2025.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Balozi Mdogo wa Oman anayefanyia Kazi zake Zanzibar Mhe. Said Salim Al Sinawi , baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid Al Fitry iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Jijini Zanzibar leo 31-3-2025.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana Mtoto Samir Idrissa, baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid Al Fitry iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Jijini Zanzibar leo 31-3-2025


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.