Habari za Punde

Mwakilishi wa Jimbo la Bumbwini Kukabidhi Vifaa na Zawadi kwa Wanafunzi Waliofanya Vizuri Masomo yao

Na. Takdir Ali.

Mwakilishi wa Jimbo la Bumbwini Mhe. Mtumwa Peya Yussuf amewataka Vijana kukiamini na kukichaguwa Chama Cha  Mapinduzi (CCM) ili kiendelee kushika Dola na kuleta  Maendeleo kwa Wananchi wake.


Ameyasema hayo hivi karibuni, mara baada ya kukabidhi vifaa vya Skuli kwa Wanafunzi waliopata Division One na Michipuo pamoja na kukabidhi Mashine za kusukumia Maji katika Jimbo la Bumbwini Wilaya Kaskazini B Unguja.

 

Amesema lengo la kukabidhi vifaa hivyo ni kuwawezesha Wanafunzi kusoma kwa bidii ili waweze kuwa Viongozi wazuri wa  hapo baadae.


Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. Mbarouk Juma Khatib amesema Chama Cha Mapinduzi kipo mstari wa mbele katika kutekeleza Ilani kwa vitendo hivyo amewataka kuendelea kukipa ushindi kwa maslahi yao na Taifa kwa ujumla.


Aidha amewasisitiza Wanafunzi kuacha mambo ya anasa na badala yake wajikite zaidi katika masomo yao sambamba na kuheshimu Wazazi na Waalimu wao.

 

Nao Wanafunzi waliokabidhiwa zawadi hizo, wameahidi kusoma kwa bidii pamoja  na kuvitunza vifaa hivyo ili viweze kuwasaidia katika masomo yao.

 

Hafla ya kukabidhi Vifaa vya Skuli kwa Wanafunzi wa Jimbo la  Bumbwini, waliopata Divition One na waliopasi Michipuo, wamekabidhiwa vitu mbalimbali ikiwemo, Photocopy Mashine, Computer, Laptop na Mashine za kusukumia Maji ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania  (UWT), Ofisi ya Zanzibar Tunu Juma Kondo.

 

                                      By Takdir Ali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.