Habari za Punde

OFISI YA TRA MBULU KUJENGWA 2026/27

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akijibu swali la  Mbunge wa Mbulu Mjini, Mhe. Zacharia Paulo Issaay, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Mbulu, jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- Wizara ya Fedha)


Na. Josephine Majura, WF, Dodoma

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amesema kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ina mpango wa kuanza ujenzi wa Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara, katika mwaka 2026/27. 

Aliyasema hayo bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbulu Mjini, Mhe. Zacharia Paulo Issaay, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Ofisi ya TRA katika Wilaya hiyo.

Alifafanua kuwa katika kipindi ambacho hakuna Ofisi ya TRA, shughuli za ukusanyaji wa mapato ya Serikali zinafanyika kwenye jengo la iliyokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.