Habari za Punde

Taasisi ya The Same Qualities Foundation ya Arusha katika kuimarisha Afya za wananchi wa Zanzibar


WIZARA ya Afya Zanzibar imesema itaendelea kushirikina na  Taasisi ya The Same Qualities Foundation ya Arusha katika kuimarisha Afya za wananchi wa Zanzibar ikiwemo kuwafanyia matibabu watu wenye midomo wazi na kuwa na muenekano mzuri.

Akizungumza mara baada ya kufanya ziara maalumu katika kambi ya matibabu ya midomo wazi inayoendelea kufanyika katika Hospitali ya mkoa Lumumba inayoendeshwa na wataalamu kutoka Taasisi ya The same qualities Foundation ya Arusha na wataalamu wa hapa nchini Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui amewataka wazazi wenye watoto walio na tatizo la midomo wazi kufika katika kambi maalumu ili kupatiwa matibabu.

Amefahamisha kuwa matibabu yanayotolewa katika kambi hiyo ni bure na dawa  zipo za kutosha na kusisitiza kuwa  wazazi washirikiane kuwatoa watoto wenye matatizo hayo  majumbani na kuwa peleka kwenye matibabu, ili kuwapatia furaha na heshima katika jamii  watapofanyiwa matibabu ya midomo yao.

Aidha amesema  katika kuimarisha huduma hizo, Taasisi hiyo imeleta madaktari bingwa wa kutibu matatizo hayo  waliotoka nchi mbali mbali kwa lengo la kuunga mkono jitihada za Serikali kupitia Wizara ya Afya Zanzibar  ambapo kila mwaka  mara mbili Unguja na Pemba wanatoa huduma hiyo.

Amesema katika kambi hiyo   matibabu hayo yatakwenda vizuri kutokana kuwepo kwa wengine waliokwenda na matatizo ya kinywa tu na kufanyiwa matibabu vizuri na wapo vizuri kiafya, wenye matatizo ya midomo wazi walipata matibabu na wamepona na kuwa na afya nzuri.

Taasi ya The Same Qualities Foundation inafanya kazi kubwa ya kusaidia jamii kwa kutoa huduma mbali mbali za Afya Tanzania Bara na Zanzibar hasa kuwapatia huduma watoto na watu wazima wenye midomo wazi na matatizo ya kinywa kambi hio imeanza  matibabu yake tangu Jumatatu Agust 25 hadi Ijumaa Agust 29 na wanatarajia kuwafanyia matibabu watu wapatao 25.

mwisho

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.