Habari za Punde

WAZIRI MKUU ASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI USHARIKA WA KKKT KISASA,DODOMA

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba akisalimiana na Msaidizi wa Askofu  wa Dayosisi  ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dodoma , Mchungaji  Stanley  Tabulu alipowasili kwenye Usharika wa  KKKT Kisasa jijini Dodoma , kushiriki ibada ya Jumapili , Novemba 16.2025. Kulia ni mkewe  Mama Neema Mwigulu Nchemba,  kushoto ni Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Daniel Sllo na wa tatu kulia ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya Dodoma,  Askofu Christian Ndosa. 
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba  akitia saini kitabu cha wageni alipowasili Usharika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Kisasa kushiriki Ibada ya Jumapili ,  Novemba 16.2025.  Kulia ni mkewe,  Mama Neema Mwigulu Nchemba

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba na mkewe Mama Neema Mwigulu Nchemba wakishiriki  katika  Ibada ya Jumapili  kwenye Usharika wa KKKT Kisasa jijini Dodoma, Novemba 16, 2025. Kulia ni Naibu Spika wa Bunge Daniel Sillo.

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba  na Mkewe Neema Mwigulu Nchemba (wa tatu kulia) pamoja na viongozi wengine wakiombewa waliposhiriki katika Ibada ya Jumapili  kwenye Usharika  wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Kisasa Dodoma, Novemba 16, 2025.  Kulia ni Naibu Spika wa Bunge, Daniel Siro.
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akizungumza katika Ibada ya Jumpili aliyoshiriki katika  Usharika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Kisasa jijini Dodoma, Novemba 16, 2025.

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba  akimsikiliza mkewe Mama Neema Mwigulu  Nchemba aliposalimia katika Ibada ya Jumapili aliyoshiriki katika  Usharika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Kisasa jijini Dodoma, Novemba 16, 2025.
Baadhi ya washiriki wa Ibada ya Jumapili katika Usharika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Kisasa jijini Dodoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba alipozungumza katika ibada hiyo aliyoshiriki, Novemba 16, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.