Hivi majuzi tumesikia uteuzi wako wa Makatibu Wakuu ambao ni watendaji muhimu wa Serikali. Kabla ya hapo tulikusikia ukituteulia Wakurugenzi kukamilisha safu ya Utendaji serikalini.
Ila kuna uteuzi ambao ni wewe pekee mwenye uwezo wa kuufanya kikatiba ila bado hatujakusikia kwani hata Rais aliyepita naye pia hakufanya. Uteuzi wa Kadhi Mkuu na Mufti Mkuu.
Tokea kufariki kwa Kadhi Mkuu Ali Khatib Mranzi, Allah Subhaanahu Wata’ala amrehemu, hadi hii leo si Rais aliyepita wala wewe hatujakusikia bado kututeulia kiongozi muhimu katika upande wa Serikali kuhusiana na mambo ya Dini.
Tokea kututoka kwa Mufti Mkuu Zanzibar ‘Allaamah Haarith bin Khelef, Allah Subhaanahu Wata’ala, amrehemu hadi hii leo hatujasikia kuteuliwa kwa Mufti mwengine.
Angalau kuna Naibu Kadhi Mkuu kwa hivyo kitengo hiki kinaweza kufanya kazi lakini hatuna Naibu Mufti Mkuu. Ila tutaendelea kwa miaka mingapi kukaimiwa na cheo hiki Muhimu cha Kadhi wakati tuna Rais aliye madarakani na tunamsikia akifanya uteuzi wa vitengo vingi vya Serikali.
Mheshimiwa Rais litupie macho suala hili kwani sijui vigezo gani hutumika katika kuwateua Waislamu wenye sifa za kuweza kuwa Kadhi na Mufti Mkuu lakini niaamini kwa busara zako utalishughulukia.
Washukran
Labels
- .
- `
- 8
- AFYA
- AFYA.
- AJALI
- BIASHARA
- BURUDANI
- DINI
- ELIMU
- FILAMU
- HABARI
- HARUSI
- HOSPITALI
- I
- JAMII
- KATUNI
- Kii
- KILIMO
- KIMATAIFA
- KITAIFA
- Ku
- MAGAZETI
- Mahkamani
- MAISHA
- MAKALA
- MAKALA AFYA.
- MAKALA.
- MATUKIO
- MATUKIO.
- MICHEZO
- MITAANI
- MIUNDOMBINU
- MSAADA
- Ok
- SIASA
- TANGAZO
- TAWA YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI
- TEKNOLOJIA
- UCHUMI
- UTAFITI
- UTALII
- VIDEO
- VIJANA
- VISA INTERNATIONAL YAZINDUA TAWI TANZANIANa Mwandishi wetu 16.07.2025DAR ES SALAAM
- WEZI
Tafsiri ya Lugha
Popular Posts
-
Dar es Salaam. 28-10-2025 Tanzania Bloggers Network (TBN) inatoa pongezi za dhati kwa Watanzania wote, wagombea, vyama vya siasa, Tume Huru ...
-
THE STATE UNIVERSITY OF ZANZIBAR (SUZA) JOB OPPORTUNITIES The State University of Zanzibar (SUZA) is the only public University in...
-
Mtaalamu wa lugha ya Alama Masika Khamis Ali akitoma maelezo kwa Wananchi wa makundi maalumu wakati wa ufungaji wa Mkutano wa Kampeni wa Cha...
-
Waziri wa Afya Zanzibar Mhe.Hamad Rashid Mohamed akitowa taarifa ya mwenendo wa maradhi ya Corona Nchini ya kuthibitika kwac Wagonjwa 23 ...
-
Na Mwandishi Wetu WMJJWM- Njombe Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Mkaundi Maaalum Dkt. John Jingu, amewataka...
-
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha ADC Mhe.Hamad Rashid Mohammed akisalimia na Viongozi mbalimbali alipowasili katika viwanj...
-
Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii ambaye ni Mkurugenzi Mkuu Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Bw. Bernard Marce...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
BLOGU RAFIKI
-
-
Rais na Mgombea wa nafasi ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan apiga Kura katika Kituo cha Ofisi ya Kijiji Chamwino mkoani Dodoma - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) M...5 days ago
-
Elimu : Bajeti za Elimu Zisipuuzwe wakati wa misukosuko ya Kiuchumi na Kisiasa Duniani - Kikwete na Malala Waonya. - Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai, wameonya juu ya mwenendo hatarishi duniani wa kupunguza au ku...2 weeks ago
-
MAHOJIANO YA TAUSI SUEDI NA AMRI NGOYE KUHUSU CSI KUPITIA KWANZA PRODUCTION NCHINI MAREKANI - Pata habari motomoto kupitia facebook kwa kulike huu ukurasa wetu https://www.facebook.com/pages/Pamojapureblogspotcom/312633955485619?ref=hl7 years ago
Marafiki Duniani
Popular Posts
-
Mwili wa Marehemu unatarajiwa kuwasili Zanzibar majira ya mchana kwa Ndege na kuendelea na taratibu za Maziko yatafanyika katika Mtaa wa...
-
The United Republic Of Tanzania National Examination Council of Tanzania Form Four Examination Results 2017/2018 The National E...
-
Makamanda wa JWTZ wakiwa wamebeba mwili wa Marehemu Waziri Kiongozi wa Kwanza wa Zanzibar na Brigedia Jenerali Mstaaf Ramadhani Haji Faki...
-
Na Miza Kona/Rahma Khamis Maelezo-Zanzibar Jumla ya wanafunzi 16,744 wamechaguliwa kuendelea masomo ya kidatu cha tatu kati ya wanafun...
-
Bwana Harusi Lusajo Sajent Mwangambaku (kushoto), akiwa katika pozi na mke wake Neema Stanley Matowe katika hafla yake ya ndoa iliyofa...
-
Mama mjazito akihangaika na hatimaye kupoteza maisha kutokana na mimba za utotoni..Video ipo hapo chini baada ya maelezo mafupi
-
Hutuba ya Mhe Waziri wa Afya Nd. Mahmoud Thabit Kombo kwa Waandishi wa Habari Katika Maadhimisho ya Siku ya Malaria Dunia Zanzibar, 22...
-
Madawa na Maji vilivyokabidhiwa na Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem, kwa Wizara ya Afya kwa ajili ya Kambi za K...

Huu ni kudhalilika kwa Waislamu. Inakuwaje ategemewe raisi kufanya uteuzi wa mufti. Hii si inaonesha kuwa serikali ina mkono katika masuala ya dini? Inakuwaje wakristo wanateua viongozi wao wenyewe lakini Waislamu bado wanamsubiri raisi. Sijui itakuwaje Zanzibar tutakapopata raisi ambae ni mkiristo.
ReplyDeleteWaislamu tukaeni chini tuchagua Mufti wetu baadae tuipe taarifa serikali.Hiyo ndio demokrasia ya kweli.
kwakumbusha tu pia kati mtendaji wakfu na mali ya amana hajachaguliwa kwa kipindi kirefu tokea afariki aliekuwepo.
ReplyDeleteAhsante mdau kwa kumuongeza Katibu Mtendaji wa Wakfu na Mali ya Amana ambye pia anakaimiwa.
ReplyDeleteNukta ya mchangiaji wa kwanza ina mantiki ni kitu ambacho ingawa leo kinaonekana hakiwezekani lakini ni suala ambalo ni Waislamu wenyewe wanapaswa kulizungumzia kwa upana faida na hasara ya kuchaguliwa Mufti, Kadhi na Serikali na kama kuna fikra mbadala ambapo kama sikosei katika miaka ya themanini iliwahi kuja fikra ya Mufti wa Waislamu wenyewe na ikapitishwa misikiti yote ya Ijumaa na kwa bahati mbaya tukasikia dhana hii pia imetekwa na serikali