Na
Rajab Mkasaba, Ikulu
WATENDAJI
na Viongozi wa Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati wameeleza kuwa
utengenezaji wa waya wa umeme unaopita chini ya bahari umekamilika na uko
njiani kuletwa Zanzibar waya ambao utalifanya tatizo la umeme linalosababishwa
na ule uliopo kuwa historia katika kisiwa cha Unguja.
Maelezo
hayo yametolewa na watendaji na viongozi hao katika mkutano kati yao na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, katika
muendelezo ya mikutano yake ya kukutaa na watendaji na viongozi wa Mawizara
yote ya SMZ katika kuangalia utekelezaji wa kazi za Wizara hiyo kwa mwaka wa
fedha 2011-2012 pamoja na vipaumbele na malengo kwa mwaka 2012-2013.
Mkutano
huo umefanyika Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na Makamu wa Kwanza wa Rais
Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi
Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Wizara hiyo ilieleza kuwa utengenezaji wa waya wa
baharini wenye kilomita 39.5 umekamilika na hivi sasa uko njia.
Meneja
Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar Hassan Ali Mbarouk, aliyasema hayo katika
kikao hicho na kueleza kuwa ulazaji wa waya huo wa pili wa chini ya bahari
kutoka Ras Kiromoni hadi Ras Fumba unatarajiwa kufanywa Agosti mwaka huu.
Alieleza
kuwa kazi hizo zote zimegharamiwa na MCC, ambapo kwa upande wa matayarisho
tayari ukamilishaji wa uwekaji wa transfoma mbili kubwa zenye uwezo wa 60MVA
kila moja tayari umeshafanywa.
Uongozi
huo ulieleza kuwa ziara ya utafiti katika eneo la mradi kutoka Ubungo hadi Ras
Fumba na Ras Fumba hadi Mtoni umeshakamilika kazi ambayo inatekelezwa na
Kampuni ya Kalpataru kutoka India.
Kampuni
ya VISCAS CORPORATION ya Japan ndio inayotengeneza waya huo pamoja na kuulaza
baharini mara utakapofika, ambapo Kampuni ya SYMBION ya Marekani ikishirikiana
na Kampuni ya
ALSTOM ya Ufaransa ndizo zinazotengeneza vituo vya kupokea umeme.
Uongozi
huo ukiongozwa na Waziri wake, Ramadhan Abdalla Shaaban ulieleza kuwa hatua
hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza kiwango cha umeme katika kisiwa cha
Unguja ili kwenda sambamba na ongezeko la mahitaji ya huduma hiyo muhimu kwa
maendeleo ya nchi.
No comments:
Post a Comment