Na Ali Issa Maelezo
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwaza wa
Rais Fatma Abdull Habib Ferej amesema pasipo kuwa na tahadhari na utaratibu mzuri wa kuvuna maliasili zisizo
rejesheka, athari mbaya za mazingira hutokea baadae bila ya kizuiwizi na kuleta maafa makubwa katika
nchi.
Hayo ameyasema leo Ofisini kwake Migombani
wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika kuadhimisha siku ya
mazingira duniani ambapo kilele chake kwa Zanzibar
itakua kesha huko visiwani Pemba .
Waziri Fereji amesema uvunaji wa mali asili zilizo mzunguka
mwanadamu na uendeshaji wa shughuli mbalimbali za kimaendeleo ni suala la
lazima kwa binaadamu yeyote ili aweze kuishi lakini iwapo binadamu hatozingatia
sheria za mazingira kunaweza kusababisha matatizo makubwa kwa wananchi na
mazingira yao.
“Uvunaji wa mali asili zilizo mzunguka
mwanadamu pamoja uwendeshaji wa shughuli
za kimaendeleo ni suala la lazima kwa binaadamu yoyote ili aweze kuishi, hata hivyo pasipokuwa na tahadhri na utaratbu mzuri wa kuvuna mali asili hizo
ndipo athari mbaya za uharibifu wa mali asili hizo na mazingira hutokea”alisema
Fereji
Aidha alisema kuwa miongoni mwa sababu zinazo
pelekea kuwepo kwa changamoto za kimazingira ni pamoja na wadau mbalimbali kutozingatia
na kufuata taratibu,kanuni na sheria zilizopo ambazo zinajikita katika
kuyalinda mazingira.
Amezitaja sheria hizo kuwa ni pamoja na
sheria za uvuvi ,misitu , aridhi na mazingira ambazo zinatoa muongozo mzuri kwa matumizi bora ya
ardhi endelevu na mali asili zilizopo katika visiwa vya Zanzibar na kusisitiza
ufuatwaji wa sheria hizo kwa faida ya
kizazi cha sasa na kijacho .
Waziri huyo alitaja athari zilizopo juu ya
mazingira ni pamoja na ukataji ovyo wa miti ya misitu, matunda na mikoko ,
ujenzi holela usio kuwa na mpangilio hasa karibu na vyanzo vya maji.
Athari nyingine ni pamoja na utupaji taka
ovyo wa taka za majumbani ,mahotelini na sehemu za biashara , uingizaji bidhaa chakavu hasa za umeme, uchimbaji mchanga, kifusi udongo, mawe na kuendelea kutumia mifuko ya plastiki.
“Mazingira ya visiwa vyetu katika hali yake
ya asili kimsingi yalikuwa mazuri yenye fukwe zenye kupendeza ,bahari iliyosheheni
rasilimali mbalimbali ,udongo wenye rutuba na miti na wanyama wa aina tofauti
,mambo yote haya yametuwezesha kufikia kwenye maendeleo tulionayo”alieleza Waziri
Fereji.
Hata hivyo waziri alisema kumekuwa na
mabadiliko ya tabia nchi ya ukame wa muda mrefu na mmong’onyoko wa fukwe athari
hizo ni baadhi ya athari nyingi za mabadiliko ya tabia nchi ambazo zimekuwa zikichangia kasi ya
upoteaji wa miti katika maeneo mbalimbali ya visiwa vya Zanzibar .
Waziri huyo alisisitiza kutunza na
kuhifadhi mazingira ili kuwa na uchumi endelevu kwa faida ya wananchi wote na
kusema kwamba suala la kuhifadhi mazingira linahitaji nguvu na juhudi za pamoja
ili kuepusha uharibifu wa mazingira na athari zake .
Maadhimisho ya siku ya mazingira duniani
hufanyika kila mwaka duniani Juni 5 ambapo kwa hapa Zanziba mwaka huu kilele chake
kitakuwa Pemba na ujumbe wa mwaka huu ni
“Uchumi endelevu jee unakuhusu wewe?”
No comments:
Post a Comment