RAMBIRAMBI
Kwa niaba ya wana-Diaspora wote
nchini Canada, Kamati Tendaji ya Zanzibar – Canadian
Diaspora Association
(ZACADIA)
inachukuwa fursa hii kutoa salamu za pole kwa wale wote waliopatwa na maafa
wakiwa katika meli iliyozama. Japokuwa tupo mbali na nyumbani lakini roho zetu
zipo pamoja nawafiwa wote na majeruhi katika msiba huu mkubwa uliyoikumba nchi
yetu.
ZACADIA
inawapa mkono wa pole wale wote waliopoteza watoto, ndugu na jamaa zao, na
kuwataka wawe na subra kwani hiyo ni miongoni mwa mitihani ya ALLAAH (SW).
Tunawatakia afya njema wale wote walionusurika na ajali hiyo.
Mola awalaze mahala pema peponi na
awape maghfira waliotangulia katika ajali hii - AMIN!
“Innaa Lillaahi wa Innaa Ilayhi
Raajiuun.”
Katibu
ZACADIA
Toronto, Canada.
No comments:
Post a Comment