Habari za Punde

Jumuiya ya watu wenye ulemavu Micheweni yaomba kutupiwa jicho

Na Salama Salim ZJMMC Pemba              

JUMUIA ya watu wenye ulemavu Wilaya ya Micheweni  Mkoa wa Kaskazini  Pemba, wameiomba Serikali na taasisi binafsi kuwapatia ruzuku  kwa ajili ya kuendeleza jumuia yao.
Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa Jumuia hio Ali Mussa Khamisi, huko Ofisini kwake Micheweni wakati alipokua akizungumza na mwandishi wa habari wa habari hii juu ya suala hilo.
Alisema kuwa serikali haina budi kushughulikia jumuia hio kwa kuwapatia ruzuku kwa lengo la kuendeleza jumuia hio kwa kuwaenua kimaslahi zaidi na kuepukana na usumbufu unao wapata kwenye jumuia yao.

Alieleza kuwa kutokana na hali ngumu ya kimaendeleo na hali za walemavu hao wanashindwa kutekeleza baadhi ya shughuli muhimu kulinganisha na uhaba wa kifedha na kukosa mitaji ya kundesha jumuia yao.
Aidha alisema kuna baadhi ya watu wasio na ulemavu kuendelea kuwanyanyapaa wanaishi na ulemavu na kuwaona kama hawana haki ya kushiriki katika shughuli zozote za kimaendeleo jambo linalowanyima fursa walemavu wilayani humo.
Alifahamisha kuwa suala la kunyanyapaliwa kwa walemavu hao linakuwa likionekana hata katika Nyanja za uongozi kutokana na ulemavu unaowakabili wanajumuia hao.
Hata hivyo aliitaka jamii kutokuwabagua watu wanaoishi na ulemavu na kuwaona kama wengine kwani ulemavu sio kifo na badala yake kuwanasihi kushirikiana kikamilifu katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo.
Kwa  upande wake mmoja kati ya wanachama wa jumuia hio Sharifa Faki Mwana alisema ipo haja kuwaona walemavu kwani tangu kuanzishwa kwa jumuia hio hakuna kitu chochote walichofaidika nacho.
“Hatuna tulicho nufaika nacho tokea kuanzishwa kwa jumuia hii kwa ajiliya kutusaidia japo katika shughuli ndogo ndogo za kutuwezesha katika jumuia”,Alisema mwanachama huyo.
Alisema jambo  zuri zaidi ni mashirikiano baina ya viongozi wa jumuia,Serikali na hata makampuni binafsi kuwasaidia ili waweze kujikwamua kimaisha na kuondokana na kuonekana kama ni watu wanaopenda kuombaomba wakati wote.
Sisi watu tunaoishi na ulemavu maisha yetu tunaonekana kama ni watu wa kuhangaika na kuombaomba watu jambo ambalo linatukatisha tama ya kimaendeleo”,alilalama mwanachama huyo.
Sambamba na hayo aliwataka viongozi wa ngazi mbalimbali kuelekeza nguvu zao kwa lengo la kuondokana na kadhia pamoja na aibu zinazoendelea kuwakumba walemavu.
Jumuiya ya watu wenye ulemavu Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, ilianzishwa mwaka 1985 na ilianza na wanachama 150 kama waanzilishi na hadi kufikia leo hii inawanachama 706 ndani ya jumuia hio.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.