WANACHAMA wa Umoja Vijana wa CCM, wametakiwa mabega yao kutowabeba viongozi wanaovuruga shughuli za serikali, na badala yake wawaumbue kwa kutowapa kura ndani ya chaguzi za Chama zinazoendelea kwa vile tayari wameanza kutembeza fedha ili kupanga safu yao.
Hayo yalisemwa jana na Mjumbe wa Kamati ya
Siasa Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja, Mama Asha Suleiman Iddi, katika ufunguzi
wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana Tanzania
Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja, ikiwa ni sehemu ya uchaguzi Mkuu wa ngazi hizo
unaoendelea kufanyika nchini kote Tanzania kupitia Chama cha
Mapinduzi.
Mama Asha, alisema UVCCM, ni moja ya Jumuiya
muhimu ndani ya Chama na haitakuwa busara kwa wanachama wake kuona wanakubali
kutumiwa kuwapitisha viongozi ambao tayari wameonesha dalili za kuvuruga
utekelezaji wa shughuli za serikali.
Alisema katika siku za karibuni baadhi ya
viongozi wameonekana kwenda kinyume na matakwa ya sera na mipango ya serikali,
jambo ambalo linaonesha kuwa hawako tayari kuisaidia serikali yao ili iweze kufikia malengo iliyojipangia .
Alifahamisha kutokana na mazingira ya
kutambulika kwa viongozi hao tayari kuna taarifa za kuanza kupanga safu ndani
ya chaguzi hizo ikiwa ni hatua ya kuwawezesha watu wanaotaka kuendelea kushika
madaraka ndani ya chama hicho.
Alisema ili kuiondoa hali hiyo ni vyema kwa
wanachama wa umoja huo, kuanza kuwaona kwa kuwanyima nafasi watazoomba kwani
baadhi yao hivi
sasa wameanza kutembeza fedha ili waweze kuchaguliwa kuingia katika uongozi.
Alisema ni lazima wachukue tahadhari hiyo
kwa vile Uchaguzi Mkuu ujao bado ni Mgumu kwa Chama cha Mapinduzi, na ni lazima
wanachama wa CCM kuona wanaowachagua ni viongozi wazuri ambao watakiwezesha
kusonga mbele.
Alisema baadhi ya viongozi hao baada ya
kuanza kujiona kuwa katika mazingira magumu kuweza kushinda katika chaguzi hizo
wameamua kutumia nafasi walizonazo kuwapangia safu kwa kuweka wagombea
wataoweza kutekeleza matakwa yao
ya kuichafua serikali.
“CCM haitaki kupangiwa safu, CCM inahitaji
wenye uchungu wa Chama na ni lazima muwaze namna ya kupata vingozi safi sio kukubali vipandikizi achaneni naoi wakija na pesa
kuleni kisha wekeni viongozi safi ”
Alisema Mama Asha.
Alisema hatari ya kuwaacha watu hao kufanya
wapendavyo kinaweza kukisababishia chama hicho kuwa katika mazingira magumu
kutekeleza majukumu yake hasa katika kuzilinda sera za Chama hicho na kuweza
kupata nafasi ya kufanya mambo yao .
Alisema vipandikizi hivyo tayari Uongozi wa
Chama cha CCM, imeanza kuwabaini kuwapo kwao katika Mkoa wa Kusini, Kaskazini,
na Mjini Unguja, ikiwa ni hatua ikiwa ni maandalizi ya viongozi hao kutaka watu
hao wapiti kwa njia yoyote ile ili waliowaweka kuweza kuwatumia kwa matakwa
yao.
Alisema maamuzi ya serikali ya Zanzibar kuingia katika
mfumo wa serikali ya umoja wa kitaifa dhamira yake ni kuona Wazanzibari
wanapata maendeleo zaidi, na amani ya nchi inakuwa, na haitakuwa busara kuona
wanawarejesha madarakani waaanaotaka kuichafua amani ya nchi.
Hata hivyo, Mama Asha aliwataka wanachama hao kuona
wanajitolea kuzifanya kazi za chama kwa kujitolea badala ya kuweka mbele
maslahi ya kuhongwa.
Aidha, Mama Asha aliwataka vijana hao
kuepuka vitendo vya vurugu juu ya hoja zinazojitokeza katika mambo ya Muungano,
na badala yake waendelee na msimamo wa Chama cha Mapinduzi na kutekeleza
Miongozo yake.
Hoja za baadhi ya viongozi kudai
hawajazaliwa na nafasi za uongozi ndani ya Chama hicho zioneshe wazi kuwa watu
hao wana lao na ni vyema wakaona umuhimu wa kuwaondoa kabla ya uchaguzi mkuu
kufika.
“Mtu anasema hataki Muungano, hataki sensa
hataki dawa ya mbu, hataki chanjo tuwaangalie hawa kwani ndo wale wale
wasiopenda Wazanzibari waendelee Chagueni mtu mwenye sura moja hatutaki vichwa
viwili kuleni pesa zeo kura kapigieni viongozi bora hakuna ataewajua” Alisema
Mama Asha.
Akiendelea alisema ni vyema kwa wanachama
hao kuona wanakaa mbali na viongozi anaoonyesha wako kwa ajili ya CCM na sio
vigeu geu.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kaskazini ‘B’
Unguja Khamis Ali, akitoa maelezo yake aliwataka vijana kuona wanachagua
viongozi ambao wataweza kukitetea Chama hicho katika uchaguzi Mkuu ujao.
“Sisitizo langu chagueni watu wazuri kufuata
muendelezo wa kazi chama kusonga mbele tumeanza kuchagua ngazi ya chini tayari
tumeshaapata viongozi wazuri sasa tunahitajiwazuri zaidi” Alisema Mwenyekiti
huyo.
Alisema waanalazimika kufanya maandalizi
hayo kwavile Chama cha Mapinduzi ndani ya mkoa huo kinajiandaa kuona Jimbo la
Nungwi linarudi katika mikono ya CCM na nguvu ya vijana ni moja ya nguzo muhimu
ya kuweza kufanikisha hilo .
Nae
Katibu wa Jumuiya hiyo Wilaya ya Kaskazini ‘B’, Salum Suleiman Tate, amewataka wanachama hao
kushirikiana na uongozi mpya utaokuja, kwa kutambua umoja huo ni tanuri kuu la
kuweza kupatikana kwa viongozi bora.
Alisema jambo la msingi ambalo wanachama hao
wanapaswa kulizingatia ni kuwa kitu kimoja na kuacha malalamiko yatayoweza
kuwagawa kutokana na baadhi ya watu wameamua kutumia dini vibaya kwa kuingiza
mambo ambayo yanaenda kinyume na matakwa ya dini.
Alisema ni lazima wanachama wa CCM kuanza
kuyaona hayio hivi sasa kwani Tanzania
imekuwa na taratibu mbali mbali za kushughulikia mambo ya dini kwa kuweka
mabaraza maalum kufanya kazi hiyo kwa vile serikali tayari haina dini ila watu
wake ndio wenyedini.
Aidha, Katibu huyo aliwataka wanachama hao
kuona wanaendelea kushiriki katika sensa pamoja na mchakato wa kupatikana kwa
Katiba mpya kwa vile bado Chama cha CCM kinahitaji kuendelea kuongoza serikali
kikiwa na katiba bora itayowawezesha Waatanzania kuishi kwa amani na utulivu..
Nae Mjumbe wa Kamanda wa Umoja huo Khamis Ali Salum, akitoa
Shukrani zake, alisema vija wa CCM Mkoa huo watahakikish wanaisaidia Serikali
kuona amanai ya Mkoa huo inaendelea kudumu kwa kuziya kutokea kwa vitendo
vyenye kuashiria kuvurugika kwa amani.
No comments:
Post a Comment