Na Nafisa Madai WMM
Msaidizi Mkurugenzi mkuu wa shirika la bandari
Pemba Hamad Salim Hamad amesema hivi sasa shirika la bandari Pemba limeweza
kupiga hatua baada ya kufanyiwa matengenezo ya gati ya Mkoani ambapo awali
ilikuwa ikituama maji.
Amesema hayo alipokua akimpa maelezo kuhusu
bandari hiyo Waziri wa Miundombinu na
Mawasilano Mhe Rashid Seif Suleiman alipofanya ziara bandarini hapo na kufanya
mazungumzo na wafanyakazi.
Mkurugenzi huyo amesema tatizo la kutuama maji
bandarini limedumu kwa muda mrefu lakini kwa sasa tatizo hilo limepatiwa
ufumbuzi yakini na limeweza kutoweka kabisa.
Akimuelezea matatizo yaliyopo kwa sasa mkurugenzi
huyo amesema shirika lake kupitia bandari ya Mkoani imekabiliwa na tatizo kreni
ambapo alisema iliyopo haiwezi kukidhi haja ya matumizi yalipo na mara nyengine
hushindwa kufanya kazi kabisa.
Aidha alisema kreni hiyo imechakaa kutokana na
kuwa na umri usiopungua miaka 28 ambapo alisema tokea kuletwa hapo mwaka 1984
inafanya kazi hadi leo.
Sambamba na hayo mkurugenzi huyo amesema shirika
lake lina mpango wa kununua kreni mpya ambayo
itamudu shughuli za bandarini hapo na isiyopungua tani 25.
Kwa upande wake Waziri wa miundombinu na
mawasiliano Rashid Seif Suleiman amesema imefika wakati kwa shirika hilo
kubadilika kiutendaji ili waweze kwenda sambamba na ushindani kwa kibiashara.
Aidha alisema wizara ya miundombinu ni wizara
ambayo inafanya kazi ya kuhudumia jamii moja kwa moja hivyo hakuna budi
kuwajengea mazingira mazuri wateja wao
Hata hivyo alishauri shirika hilo kufanya
mazungumzo na wafadhili ili waweze kuwajengea turubali katika njia inayopita
abiria wakati wa kwenda kupanda meli kwani masafa ni marefu sana.
waziri huyo amesema kuanzia sasa shirika hilo
kushirikiana na ZMA kuandaa utaratibu maalumu wa kupima uzito wa gari
zinazoingia gatini ilikuepusha kuharibu miundombinu iliyopo.
Hata hivyo alisema gari ambayo itabaanika kuvunja
miundombinu ya gati hiyo itachukuliwa hatua za kisheria kwa vile watakua
wamekiuka utaratibu uliopo.
Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa shirika
hilo Salim Said amesema ni vyema
serikali ikishirikiana na wizara ya miundombinu kutafuta chombo cha uokozi kwani
amesema bandari zote tatu hazina kifaa hicho
Aidha amesema watendaji wa shirika hilo kwa
upande wa Pemba wanahitaji kuboreshwa kwa kupatiwa vitendea kazi pamoja na
kuboreshwa kwa bandari yenyewe.
Kabla ya kufanya Ziara Bandarini hapo Mhe Rashid
alitembelea maendeleo ya barabara ya kipitacho
yenye urefu wa kilomita 1.6 bonde
la mpunga wilaya ya Mkoani mkoa wa kusini Pemba.
Mhe Rashid alipatiwa maelezo kuhusu
maendeleo ya barabara na mhandisi mkaazi Khamis Masoud ambapo alisema hatua ya
ujenzi umefuatiwa agizo la mhe Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein na
utekelezaji wake umefanikiwa asilimia mia moja.
No comments:
Post a Comment