Habari za Punde

UAMSHO washauriwa kufanya biashara


Nkyandwale Franco, Sumbawanga
KIKUNDI cha wanawake wajasiriamali  cha UAMSHO kilichopo katika Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa, kinachojumuisha wanawake wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa na wale taasisi binafsi kimeshauriwa kufanya biashara zao kitaalam  kwa lengo la kuongeza zaidi.

Ushauri huo umetolewa na mmoja wa wanakikundi hao ambaye pia ni Mkurugenzi  wa Chuo Kikuu Huria tawi la Rukwa, Dk. Elna Lyamuya mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya kuitisha kikao cha pamoja cha watendaji wake wa kike  kilicholenga kuunda kikundi hicho.


Dk. Lyamuya alisema ili wanawake hao waweze kujikomboa na kufanya biashara zao kuendana na kasi ya mabadiliko ya kitenolojia ni lazima wajikite katika elimu itakayowasaidia kunufaika na biashara wanazozifanya zikiwemo zile za usindikaji vyakula,uuzaji wa nafaka pamoja na zile ufugaji wa kuku na ng’ombe wa kisasa.


Wanawake hao pia wameshauriwa kufanya mchakato wa bidhaa zao kuanzia kuzalisha hadi kufikia hatua za uuzaji   kwa lengo la kuwafanya wao waweze kufahamika kibiashara bila kusahau kuboresha ubora wa bidhaa zao.

Awali katika kikao hicho Mkuu huyo wa Mkoa alisema lengo la kuunda umoja huo unaolenga kuelimisha wanawake wengine kuondokana  na dhana tegemezi ni  kuwasaidia wanachama katika masuala ya elimu.

Mara baada ya kikao hicho, wanawake hao waligawiwa kanga zilizotolewa na Mkuu wa mkoa  kama kumbukumbu ya uanzishili wa chama hicho.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.