Othman
Khamis Ame
MJUMBE
wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Balozi Seif Ali Iddi amesema
sifa sahihi watakayoendelea kupewa wazazi
popote walipo itapatikana endapo jukumu
la kuwalea watoto wao watalipa kipaumbele kinachostahiki.
Balozi
Seif ambaye pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alifahamisha kwamba mfumo wa
utandawazi wa dunia uliopo hivi sasa
umechangia kuathiri malezi bora ya vijana
ndani ya jamii licha ya kwamba upande mmoja unaelimisha.
Akiufungua
mkutano mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Kaskazini Unguja katika ukumbi wa mikutano
wa ofisi ya CCM jimbo la Kitope, Balozi Seif alisema jumuiya hiyo hivi sasa ina kazi nzito ya
malezi ya vijana kutokana na mfumo wa utandawazi.
Balozi
Seif alionya kwamba baadhi ya wazazi nchini wanahusika katika janga la upotofu
wa maadili kwa vijana kutokana na kuwaridhia watoto wao kupindukia na matokeo
yake watoto hao kukosa heshima kwa kiwango cha kutisha.
“Utandawazi
kwa kiasi kikubwa umeharibu mfumo wa malezi na kupelekea baadhi ya watoto
kuwaita baba zao madingi wakati mama wakiwaita mom. Sasa tunakwenaa wapi,?” alihoji Balozi Seif .
“U
dot. com wao walioubeba vijana hivi sasa unawaharibia maadili yao. Sasa watoto wetu heshima zao zimepungua
kutokana na utandawazi uliotuharibia mfumo wetu wa malezi,”alieleza.
Alisema
wanajumuiya hiyo lazima wawadhihirishie wananchi, CCM na vijana wote kwamba jumuiya
hiyo ina nguvu kwa vile inabeba watu wa rika zote katika jamii inayowazunguuka.
Balozi
Seif aliwashauri viongozi wapya watakaochaguliwa katika mkutano huo kukubali
kubeba dhamana ya kuwa waaminifu, waadilifu na upendo ili kuisaidia serikali kuu
kwa wao ndio walezi katika kutoa elimu kwa watoto.
Akizungumzia
suala la amani Balozi Seif aliitaka jamii kupiga vita dalili zote zinazoashiria
kuvurugika kwa amani ambayo ikitoweka hakutakuwa na wakati wa kujenga uchumi wa
taifa.
Aliwakumbusha
viongozi wa jumuiya hiyo na wanaCCM
kuendelea kuisimamia amani iliyopo nchini kama
ilani ya chama hicho ilivyoelekeza.
Aliwakumbusha
wanaCCM wote kuendelea kutetea sera na ilani za chama chao bila ya kificho kwa
vile wanaziamini na walishiriki katika kuzitengeneza.
Mapema Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa
Kaskazini Unguja ambae pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania
upande wa Zanzibar, Mussa Ame Silima alisema jumuiya hiyo inaendelea kufanya
chaguzi zake katika ngazi mbali mbali sambamba na jumuiya nyengine kutokana na
mabadiliko ya ngazi za juu ya CCM.
No comments:
Post a Comment