Na Mwandishi wetu
KATIBU
Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Ban Ki-moon amepongeza hatua ya amani na utulivu
uliofikiwa Zanzibar
kufuatia maridhiano na makubaliano ya kisiasa visiwani humo.
Ki-moon
alitoa pongezi hizo alipokutana na Rais Jakaya Kikwete, katika makao makuu ya
UN mjini New York,
Marekani.
Katibu
Mkuu huyo alimwambia Rais Kikwete kuwa sasa Tanzania
na eneo lote la Afrika Mashariki linanufaika na uamuzi mwingine wa busara wa
kisiasa wa kutafuta na kupata maridhiano Zanzibar.
Aidha
Ki-moon amesifu na kupongeza uamuzi wa Rais Kikete wa kuridhia mageuzi ya katiba
ya Tanzania.
“Nakupongeza
sana kwa uamuzi wako sahihi na wa busara wa kisiasa wa kuangalia upya katiba ya
sasa ya nchi yako kwa nia ya kutungwa kwa katiba mpya kwa sababu hatua hiyo
dhahiri itaendeleza utulivu ambao umedumu Tanzania kwa miongo mingi,” alisema Ki-moon.
Rais
Kikwete ambaye yuko New York, Marekani, kwa ziara ya siku mbili amekutana na
Ban Ki Moon ikiwa ni shughuli yake ya kwanza rasmi tokea alipowasili mjini humo
mchana wa juzi.
Katibu
Mkuu huyo wa UN amesifu jitihada zinazofanywa na viongozi wa nchi wa eneo la
Maziwa Makuu katika kuleta amani Mashariki mwa Congo (DRC).
“Niliitisha
mkutano wa viongozi wa eneo hilo Septemba 27, mwaka huu, walihudhuria viongozi
wengi akiwamo Rais Joseph Kabila wa DRC na Rais Paul Kagame wa Rwanda, na kuwaeleza
kuwa Umoja wa Mataifa unafuatilia kwa makini matukio ya eneo hilo na
kuwajulisha kuwa kama wanahitaji msaada wowote basi sisi tuko tayari,” alisema
Ki moon.
Katibu
Mkuu huyo pia alimwomba Rais Kikwete kusaidia maendeleo ya kisiasa nchini Zimbabwe
kufuatia Rais Kikwete kuchaguliwa Mwenyekiti wa chombo maalum cha Jumuia ya
Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kuhusu siasa, ulinzi na usalama.
“Kwa
nafasi yako kama Mwenyekiti wa chombo maalum cha SADC ni dhahiri kuwa unaweza
kuchangia sana maendeleo ya kisiasa ya Zimbabwe,” Ki-moon alimwambia Rais
Kikwete.
Rais
Kikwete alimweleza Katibu Mkuu huyo kuwa uamuzi wa kuunda katiba mpya unalenga
kuwa na katiba ambayo itaiongoza Tanzania kwa miaka 50 ijayo.
“Baada ya kutumia katiba yetu nzuri kwa miaka
50 iliyopita, tukaamua kuwa pengine ni vyema kuunda katiba ambayo itatupeleka
kwa miaka mingine 50 ijayo,” alisema.
No comments:
Post a Comment