Habari za Punde

Dk.Shein Awasili Nchini Vietnam Leo

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Maofisa wa Serikali ya Vietnam, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam, akiwa katika ziara rasmi ya Kiserikali

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekitri wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed  Shein,(katikati) akifuatana na mwenyeji wake Kiongozi Mkuu katika Ofisi ya Rais Ikulu Nchini Vietnam, Bw Giang Son,(wa pili kushoto) baada ya mapokezi rasmi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam,akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali,(kushoto) Balozi wa Tanzania Nchini China,pia akiwakilisha nchini Vietnam Philip Sang'ka Marmo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekitri wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed  Shein, akiteta jambo na  mwenyeji wake Kiongozi Mkuu katika Ofisi ya Rais Ikulu Nchini Vietnam,Bw Giang Son,wakiwa katika ukumbi wa Mapunziko  VIP  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam,akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali
Mama Mwanamwema Shein,(kulia) Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman,(atikati) na Balozi wa Tanzania Nchini China,pia akiwa anafanya kazi zake nchini Vietnam, Philip Sang'Ka Marmo,wakiwa katika Chumba cha Mapumziko  VIP  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hanoi Nchini Vietnam,wakiwa ni miongoni mwa Ujumbe wa Rais wa Zanzibar Nchini Vietnam

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.