Habari za Punde

Kikao cha Baraza kuanza Kesho.



MISWADA minne ya Sheria inatarajiwa kuwasilishwa na kujadiliwa katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachotarajiwa kuanza leo huko Chukwani nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Yahya Khamis Hamad, alisema hayo jana katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ofisi za Baraza hilo.

Aliitaja miswada itakayowasilishwa kuwa ni pamoja na mswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya usafiri wa baharini nambari 5 ya mwaka 2006.

Mswada mwengine ni wa sheria ya kuanzisha Shirika la Utangazaji Zanzibar, Kazi, Majukumu na Utawala wake pamoja na mambo mengine yanayohusiana na hayo.

Katibu huyo wa Baraza alisema pamoja na mambo mengine lakini pia kikao hicho kitapokea mswada wa Sheria ya kunzisha Shirika la Meli Zanzibar, Kazi, Uwezo na mambo mengine yanayohusiana na hayo.

Aidha mswada mwengine ni pamoja na sheria ya marekebisho ya Sheria ya Marekebisho ya sheria ruzuku kwa vyama vya siasa nambari 6 ya mwaka 1997 na mambo ynayohusiana na hayo.

Sambamba na hilo lakini pia Baraza hilo litapokea ripoti ya kamati Teule ya kuchunguza utendaji wa Shirika la Umeme Zanzibar.

Kikao hicho kinatarajiwa kuwa cha wiki mbili pia kitaweza kuwa na maswali na majibu 117 ambayo yataulizwa na wajumbe wa Baraza hilo na kujibiwa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.