Na Pascal
Buyaga,Mara
WATU
saba wamefariki papo hapo na wengine zaidi ya 47 kujeruhiwa vibaya baada ya
mabasi mawili ya abiria kugongana uso kwa uso.
Miongoni
mwa waliofariki ni wanawake wanne na wanaume watatu
Ajali
hiyo mbaya kuwahi kutokea katika mwaka huu, ilitokea katika kijiji cha
Nyatwari, tarafa ya Serengetu wilayani Bunda mkoani Mara.
Ajali
hiyo iliyahusisha mabasi ya kampuni ya Mwanza Coach aina ya scania marcopolo
lenye namba za usajili T756AWT mali
ya Halfan Ahmed ambalo lilikuwa
likitokea Musoma kuelekea Mwanza na basi la kampuni ya Bestline lililokuwa likitokea Mwanza kuelekea Sirari
wilayani Tarime.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara, Absalom Mwakyoma
alisema kuwa ajali hiyo ilitokea majira
ya saa 11 jioni katika eneo ambalo barabara kuu inafanyiwa matengenezo, hivyo
kuwepo vumbi jingi kiasi cha madereva kushindwa kuonana.
Mwakyoma
alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa mabasi hayo na madereva
kutokuwa makini.
Majeruhi
wamekimbizwa katika hospitali ya wilaya Bunda kwa matibabu.
Aidha
alisema majeruhi 14 ambao hali zao ni mbaya wamepelekwa katika hospitali ya
rufaa ya Bugando kwa matibabu zaidi.
Baadhi
ya abiria walikuwemo kwenye mabasi hayo walisema mabasi hayo yalikuwa yakiendeshwa
kwa mwendo wa kasi na licha ya kuwataka madereva wapunguze mwendo lakini
hawakusikilizwa.
No comments:
Post a Comment