Na
Kija Elias, Kilimanjaro
WAHAMIAJI
haramu 21 kutoka nchini Ethiopia
wamekamatwa na
polisi
mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.
Akithibitisha
kukamatwa kwa wahamiaji hao kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boaz,
alisema walikamatwa
Januari
12 mwaka huu majira ya 7:30 usiku wilayani Same mkoani hapa.
Boaz
alisema wahamiaji hao walikatwa na polisi waliokuwa doria ambapo walikutwa
katika gari lenye nambari za usajlii T
773 ALA Toyota
land Cruser lililokuwa likiendeshwa na dereva aliyetambulika
kwa
jina la John Malamla (28).
Alisema
jeshi hilo kwa
kushirikiana na idara ya uhamiaji watawafikishwa mahakamani mapema iwezekanavyo
wahamiaji hao ili kujibu mashitaka yanayo wakabili.
Kufutia
tukio hilo kamanda huyo,alitoa wito kwa wananchi kushirikiana na jeshi hilo ili
kubaini mtandao wa watu wanaowaingiza nchini humo kinyume cha utaratibu kwani
ni hatari kwa maisha yao.
Alisema
uhamiaji haramu limekuwa tatizo kubwa mkoani hapa na kwamba, kuna
mtandao
wa watu wanajihusisha na biashara ya kuwasafirisha kutoka Kenya.
Alisema
watu hao hawawezi kupita mpakani na kuingia mkoani bila kuwa na watu wanaowaongoza,
na kwamba wanachokifanya ni kuchunguza mtandao mzima wa watu wanaowaingiza
nchini kinyume cha sheria za uhamiaji.
No comments:
Post a Comment