Na
Khamis Haji,OMKR
MAKAMU
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amemtaka mfanyabiashara
aliyeingiza Zanzibar tani 781 za unga wa ngano usiofaa kwa matumizi ya
binaadamu ambao bado upo bandarini Malindi kuuondoa katika kipindi cha mwezi
mmoja kuanzia jana.
Maalim
Seif ametoa agizo hilo
alipotembelea bandarini Malindi kwa ajili ya kupata maelezo ya utekelezaji wa
agizo la serikali la kuondolewa unga huo.
Alisema
unga huo lazima uondoke bandarini kwa sababu taasisi zilizofanya uchunguzi
zimeugundua kuwa ni hatari kwa matumizi ya binaadamu, na kwa mujibu wa sheria
bidhaa kama hizo hutakiwa zirejeshwe
zilikotoka.
“Natoa
mwezi mmoja, kuanzia leo hadi Februari 13 wahusika mhakikishe unga huu
umeondolewa Zanzibar,” aliagiza Maalim seif.
Unga
huo wa ngano uliingizwa Zanzibar kutokea nchini Uturuki na kampuni ya Bopar
Enterprises mwezi April mwaka jana, lakini tokea wakati huo bado haujaondolewa
na hivi sasa umeanza kutoa harufu kali.
Maalim
Seif alieleza kuwa serikali ya Mapinduzi
Zanzibar haina muhali katika suala la kulinda afya za wananchi, kwa sababu
vyakula visivyofaa vinasababisha hatari kubwa kwa afya za binaadamu.
Katika
ziara hiyo ya Maalim Seif bandarini hapo, kampuni ya Bopar pamoja na kampuni ya
uwakala wa meli iliyoleta unga huo zilionekana kuvutana,huku kila upande ukiutupia
lawama upande mwengine kuwa ndio unaostahili kubeba lawama.
Hata
hivyo, Maalim Seif alisema lazima wahusika wawajibike kwa mujibu wa sheria
katika kulinda afya za wananchi, lakini pia waondoe msongamano katika bandari
hiyo, ambapo nafasi yalipo makontena 30 yenye unga huo inahitajika kuwekwa
mizigo mingine.
Mrajis
wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi, Dk. Burhan Othman Simai ambaye alikuwepo
katika ziara hiyo, alisema bodi hiyo imegundua kuwa unga huo haufai kwa
matumizi ya binaadamu, na kwa mujibu wa sheria mhusika anapaswa kuurejesha
ulikotoka.
Hata
hivyo, alieleza kuwa pamoja na kwamba sasa ni muda mrefu tokea kutolewa maamuzi
ya bodi kuhusu bidhaa hiyo, wahusika wameshindwa kutekeleza.
Aliwataka
wafanyabiashara wote kuhakikisha wanaingiza bidhaa ambazo ni salama na
hazitaleta athari zozote za kiafya kwa watumiaji wake.
Kamati
ya Mawasiliano na ujenzi ya Baraza la Wawakilishi pia iliagiza unga huo uondolewe
wakati ilipotembelea bandari hiyo mwezi Novemba.
Hivi
karibuni tani nyengine 325 za mchele mbovu aina rainbow na kitumbo
unaomilikiwa na mfanyabiashara Mohammed
Salum Alaiy ulingizwa nchini ukitokea nchini India na Srilanka.
Tayari
Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi imeshaagiza unga huo urejeshwe ulikotoka
lakini hakuna hakika kama agizo hilo
tayari limetekelezwa.
Raisi anafanya nini Ikiwa Watu hao hawataki kutii Amri ya Bodi. Tunataka Kiongozi na Serikali itakayoheshimika.
ReplyDeleteNyie mmewapa mwezi mmoja, Mhe Mwakyembe aipa meli masaa 24 iondoke kwa kuleta mafuta chini ya kiwango
ReplyDeleteTusubiri huo mwezi tuone!