Habari za Punde

Mchezo wa GOJU-RYU Karate yapata Viongozi Wake.



JUMUIYA ya Mchezo wa GOJU-RYU KARATE Zanzibar hatimai yapata viongozi wake katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika katika ukumbi wa Judokan Amaan. Jumuiya hiyo kwa muda mrefu ilikuwa  na Uongozi wa muda.

Kwa mujibu wa Msimamizi wa Uchaguzi huo amesema uchaguzi huo umefanyika kwa taratibu zote za Katiba ya Jumuiya hiyo na kupata Viongozi wake kwa kupitia uchaguzi huo, ambao ulikuwa na mvutano kwa panda za Nafasi za Mshika Fedha na Katibu Mkuu.

Uchaguzi huo umesimamiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Karate  Taifa Zanzibar, Haji Hassan Hussein, amesema uchaguzi huo umefanyika kwa haki za taratibu zote za Katiba ya Jumuiya hiyo na kupata Viongozi halali watakaogozi Jumuiya hiyo kwa muda wa miaka minne.
zilikuwa
Amesema katika nafasi zilizongombewa katika jumuiya hiyo ni nafasi ya Mwenyekiti  ambayo haikuwa na mpizani ilikuwa na mgombea Hamad Suleiman, ambaye ameshinda kwa kura 15,na kura mbili zimeharibika, kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Unguja ameshinda Salum Amuor Nassor kwa kura 16,na kwa Pemba ameshinda Ridhiwan Mohammed Salum kwa kura 14.


   Kwa nafasi za Katibu Mkuu na Mshika fedha zilikuwa na upinzani kwa wagombea wake kwa baadhi ya wagombea kututimiza masharti ya Katiba ya Jumuiya hiyo.amesema nafasi hiyo ya Katibu Mkuu imechukuliwa na Haji Kombo Faki kwa kura 13, na mpizani wake Said Seif Abdalla amepata kura 3.Msaidizi Katibu Mkuu Unguja imechukuliwa na Mohammed Nour kwa kura 15 na kwa Pemba imechuliwa na Khalfan Suleiman kwa kura 16.

Amesema kwa nafasi za Mshika fedha wagombea wake wamechuana vikali na kuibuka mshindi kwa kura chache na kuibuka mshindi Yusuf Abrahaman Najim kwa kura 8 dhidi ya mpizani wake Hamadi Juma Said amepata kura 7, na kwa upande wa Mshika Fedha Msaidizi Unguja imechukuliwa na Ramadhani  Rashid Mohammed kwa kura 15 na kwa Pemba imeshikiliwa na Abdalla Omar Ali.

Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Karate Taifa Zanzibar Haji Hassan Hussein amewashukuru washiriki wa uchaguzi huo na kuwapongeza Wajumbe wate wa Mkutano Mkuun wa Jumuiya hiyo kwa utulivu wao wakati wote wa uchaguzi hati tamati ya shughuli hiyo na kuwapata washindi.

Amewataka washindi wa uchaguzi huo kufanya kazi zao kwa umoja ili kuivusha Jumuiya hiyo katika mashindano yake ya Ndani na Njee ya Zanzibar wakati wa ushiriki wake na kukipa mafanikio katika kipindi chao cha uongozi.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.