Habari za Punde

Mwakilishi Bububu Hussein BHAA Aongeza Basi kwa Wanafunzi wa Jimbo lake.




Mwakilishi wa Jimbo la Bububu Hussien Ibrahim  Makungu (BHAA) ameongeza basi jengine kwa ajili ya kutowa huduma ya Usafiri kwa Wanafunzi wa Jimbo lake kuondosha kero ya usafiri kwa Wanafunzi inayowakabili wanafunzi katika Visiwa vya Zanzibar.

Amesema ameamua kuongeza basi jengine baada ya kuona  basi lililokuweko  halitoshi kwa wanafunzi hao.

Hayo ameyaeleza leo wakati akiwa katika kituo cha daladala darajani wakati akikabidhi basi hilo kwa wanafunzi wanaotoka skuli mchana na kuanza kutowa huduma hiyo na kufanya idadi ya mabasi kuwa  mawili yakitowa huduma hiyo kuanzia leo.


Amesema hayo aliyokuwa amewaahidi Wananchi wa Jimbo lake wakati wa uchaguzi anayatimiza na ikiwemo kukimalizia ujenzi wake kituo cha afya Mwanyanya na kuyaimarisha matawi ya CCM katika jimbo hilo kwa kuyawekea umeme na kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo la bububu na kupiga hatua mbele katika maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Nae Mwenyekiti wa  CCM  wa Mkoa wa Magharibi Yussuf Mohammed  amempongeza Bhaa kwa jitihada zake na utendaji wake uliochukuwa muda mfupi kutimiza ahadi alizozitowa wakati wa kampeni yake katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, na alipoingia madarakani ametekeleza ahadi zake kwa kiasi kikubwa  kwa kutowa vifaa mbalimbali katika jimbo lake na kumtaka kuendelea na juhudi zake kuliletea jimbo hilo maendelea zaidi.


Tujenge wivu wa kimaendeleo na tusijenge uchoyo na ubinafsi ,alisema Yussuf na kuwasihi viongozi hao.

Amewataka Wananchi vifaa hivyo wavitunze kama inavyotakiwa pia amesisitiza kudumisha umoja na mshikamano katika jimbo lao ambalo litaweza kukiendeleza Chama hicho.

Amesema  Napenda kuwaona viongozi wanaowajibika kiujasiri na watendaji katika chama,kitu ambacho kitaweza kupiga hatua nzuri katika chama amesema.

Vilevile amekishauri Chama kutengeneza mbinu mbadala ya kuweza kuleta mapato sambamba na kinamama kuazisha miradi ya na vikundi vya ushirika katika jimbo hilo na kuweza kujitegemea kiuchumi.

Ziara ya wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Magharibi kwa wilaya ya Mfenesini imeanza januari 15,mwaka huu ilimalizia mwishoni mwa wiki hii katika jimbo la bububu , ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Magharibi Yussuf Mohammed Yussuf, iliyoanza kutembelea jimbo la Dole, Mtoni na Bububu kwa lengo la kuimarisha Chama cha Mapinduzi katika Mkoa huu.

1 comment:

  1. Hongera Mwakilishi wangu, nadhani wengine waige mfano wake, umeonesha njia kwa kuanza kutekeleza ahadi zako. Nadhani sasa tufike wakati tumchaguwe mtu kwa kigezo cha kutekeleza ahadi zake, usiwe na wasiwasi kwa staili hii utakuwa muwakilishi wetu wa kudumu hatuna cha CUF wala CCM, sisi wengine hatuangalii chama ila utendaji wa kiongozi mwenyewe.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.