Masanja Mabula,Pemba
SERIKALI ya Wilaya ya Wete imevishtukia vitendo vinavyofanywa na baadhi ya
wananchi walio nje ya kisiwa cha Pemba wanaoingia ndani ya wilaya hiyo na kudai
kuwa mashamba ya mikarafuu yanayomilikiwa na serikali kuwa ni mali yao.
Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa wilaya hiyo, Omar Khamis Othman amewaagiza Masheha wote kuyaorodhesha mashamba
yote ya serikali na kuyawasilisha ofisini kwake.
Alisema katika kipindi baada ya
karafuu kupandishwa bei kumeibuka watu kutoka ndani na nje ya wilaya hiyo
wanaodai kuwa mashamba yaliyogawiwa kwa wananchi mara baada ya Mapinduzi ni
mali yao.
"Tumepokea taarifa kutoka kwa Masheha wakisema kumekuwepo baadhi ya
wananchi wanaodai mashamba yaliyogawiwa
eka tatu tatu na serikali ni yao , hili sisi hatuwezi kulivumilia na tayari n
tumewaagiza Masheha kuwa macho na watu wa aina hiyo,"alisema Mkuu huyo wa
wilaya wakati akizungumza na gazeti hili.
Amezitaja Shehia ambazo vitendo hivyo vimejitokea kuwa ni shehia ya Mtambwe
Kaskazini na Kusini , Pandani na Kambini
Shehia ambazo karafuu zinaonekana
kuzaliwa kwa wingi.
Aidha alisema wananchi ambao wanatuhumiwa kuwakabidhi watu hao mashamba, wajue kuwa wamekwenda
kinyume na sheria kwani walitakiwa kuyakabidhi kwa serikali kwanza kabla ya
kuchukua hatu hiyo.
Hata hivyo alifahamisha kuwa wapo baadhi ya watendaji wa Idara ya Ardhi
Pemba ambao wamekuwa wakichohea hali hiyo, lakini bado serikali ya wilaya inaendelea
kufanya uchunguzi na wakibainika watawatolewa taarifa kwa viongozi wao.
Naye Sheha wa Pandani, Said Hamad
alisema iwapo masheha hawatakuwa makini juu wa watu hao , basi wananchi
waliopewa mashamba na serikali watakosa sehemu ya kulima kufuatia na nyaraka
bandia wanazotoa watu hao.
Aliwataka Masheha kuwa makaini na kutokubali kutokea kwa vitendo hivyo
katika maeneo yao, na kwamba wawe waangalifu na wepesi wa akutoa taarifa katika
ofisi za wilaya ili hatua za haraka zichukuliwe.
No comments:
Post a Comment