Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
WAZIRI wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe ameagiza
kukamatwa maafisa kadhaa katika Bandari ya Dar es Salaam kutokana na kutuhumiwa
kuhusika katika wizi wa madini ya tanzanite kutoka Rwanda.
Dk. Mwakyembe alisema katika kipindi cha miezi minne
serikali imekuwa ikipokea malalamiko kutoka serikali ya Rwanda juu ya wizi wa
madini hayo unaofanywa katika bandari hiyo.
Hatua ya Waziri huyo ni muendelezo wa mkakati wake wa
kuisafisha bandari hiyo ambayo imekimbiwa na wafanyabiashara wengi kutokana na
kuwepo ufisadi.
Hivi karibuni Waziri huyo alimfukuza kazi Mkurugenzi Mkuu
wa Mamlaka ya Bandari (TPA) pamoja na wasaidizi wake kutokana na utendaji mbovu
na ubadhirifu uliosababisha serikali kukosa mapato.
No comments:
Post a Comment