Habari za Punde

Polisi wafunzwa lugha za alama



Na Kauthar Abdalla
AFISA mradi wa kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto kutoka shirika la Action Aid, Nadra Subeit Ali amesema mafunzo ya lugha za alama kwa  askari polisi yana umuhimu katika utendaji wa kazi zao kwani yatapunguza masuala ya ukatili wa watoto.

Akizungumza na mwandishi habari mara baada ya mafunzo hayo katika ukumbi wa elimu mbadala Rahaleo, alisema kumekuwa na matukio mbali mbali ya ukatili kwa watoto viziwi na hali ambayo inapelekea kukosekana kwa ushahidi.

Alisema watoto wenye ulemavu hufanyiwa mambo ambayo hayastahiki kufanyiwa katika jamii lakini jambo la kusikitisha wanashindwa kwenda kuripoti katika vituo vya polisi kutokana na tatizo la mawasiliano.


Aidha alisema malengo makuu ya kuandaliwa mafunzo hayo kwa askari ni kuwafanya wawe karibu na waathirika wa vitendo hivyo kwani ndio wanaopokea kesi kwa mara ya kwanza na kushindwa kuwasiliana nao.

Alifahamisha kuwa watajitahidi kutafuta kila mbinu ili kuhakikisha watu wenye ulemavu hasa wa vziwi wanapata haki zao za katika sehemu mbali mbali ikiwemo katika vyombo vya sheria.

Nae Mkuu wa Dawati la jinsia polisi Madema, Zahor Faki Mjaka alisema mafunzo ya lugha kwa askari yana umuhimu kwa sababu ya wateja wanaowapata huwa wana mahitaji maalum na wanashindwa kuwasiliana nao hadi watafute wakalimani kutoka sehemu nyengine.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.