Na Abdi Suleiman, Pemba
WANANCHI wa Jimbo la Ziwani
Mkoa wa Kusini Pemba, jana walifunga safari hadi zilipo ofisi za Wizara ya
Katiba na Sheria Pemba kwenda kuwasilisha malalamiko yao juu ya kuwepo kundi la
vijana linalopita vijiji mbali mbali vya jimbo hilo, kutangaza na kueneza
madhebu ya shia, ambayo wao wanayapinga vikali.
Wakizungumza mara baada ya
kufika wizarani hapo, wananchi hao kike kwa kiume, walisema vijana hao wamekuwa
wakihamasisha ndoa za muda mfupi (Muta’aa) na kulawiti.
Walisema kuhalalisha liwati
na ndoa za muda mfupi ni kinyume na maarisho ya Mwenyezi Mungu na kusema tayari
kuna baadhi ya watoto wao wameanza kufuata madhehebi hayo.
“Wanapita kila kijiji na kuhalalisha ndoa za
muda mfupi na kulawitiana kwa watu walio kwenye ndoa vitendo ambavyo ni haramu
katika imani ya kiislamu,” walisema.
Walionya kuwa vijana hao
wasipopigwa vita, wanaweza kusababisha udhalilishaji mkubwa wa kijinsia na
kingono hasa kwa wanawake walio kwenye ndoa.
Mmoja kati ya wananchi
hao,Tatu Khamisi Bakari, aliiomba wizara
ya Katiba kupitia ofisi ya Mufti kulitolea ufafanuzi suala hilo na kuwaondosha
haraka vijana hao kabla hawajachukua hatua za kuwaondoa kwa nguvu, jambo ambalo
linaweza kusababisha vurugu.
Mohammed Mussa
Juma, ambae ni mwanakijiji
wa Ziwani, alisema vijana hao
wamekuwa wakiwatumia zaidi watoto walio na umri kuanzia miaka 15-20, ambapo
huwachukua kutoka kwa wazazi wao na kuwasafirisha hadi Dar es Salaam kwa madai
ya kwenda kuwafundisha uislamu lakini badala yake huwafundisha ushia.
Alisema tayari kuna vijana
wengi wa kijiji hicho walioko Dar es Salaam kufundishwa madhehebu hayo, na
kuiomba serikali kufanya liwezekanalo kuhakikisha vijana hao wanarejeshwa.
Mkuu wa Makosa ya Jinai na
Upelelezi wa polisi, Wilaya ya Chake Chake, Ali Mzee, alisema hitilafu za
kidini zinashughulikiwa na ofisi ya Mufti, hivyo aliwataka wananchi wa Ziwani, kuwa tayari kutetea haki zao ofisi ya Mufti na
kuepuka kufanya vitendo vinavyoweza
kusababisha vurugu.
Alisema madhehebu ya Suni na
Shia, yote ni madhehebu ya kidini hivyo hawapaswi kutafarukiana.
Naye Kaimu Msaidizi Mufti
Pemba, Abrahamani Abdalla Naamani, amewahidi wananchi hao kwamba madai yao yatafikishwa katika ofisi ya Mufti Mkuu
wa Zanzibar, kwa kufanyiwa kazi.
Aliwasisitiza wananchi hao
kuwa na umoja na mshikamano, katika kulipatia ufumbuzi tatizo hilo, na
wasichoke kufuatilia.
No comments:
Post a Comment