Na himid Choko, BLW
SPIKA wa
Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, Pandu Ameir Kificho amesema Wajumbe wa
Baraza hilo hivi sasa wako makini zaidi
baada ya kujengewa uwezo mkubwa wa kiutendaji
chini ya Ufadhili wa Shirila la
Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Amesema
kwa kipidi kirefu UNDP kupitia miradi
tofauti ya Kusaidia Mabunge , imeweza kusaidia kutoa taaluma ya utendaji wa vyombo hivyo hapa nchini.
Amesema
kwa upande wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, chini ya miradi hiyo limekuwa likifaidika kwa mafunzo ya ndani na
nje ya nchi kwa Wajumbe wa Baraza hilo
pamoja na watendaji .
Aidha amesema UNDP kwa kiasi kikubwa imesaidia
vitendea kazi ndani ya Baraza
hilo ikiwemo Usafiri.
Spika
Kificho amesema hayo leo wakati akizungumza
na Naibu Mkurugenzi Mkaazi wa UNDP hapa nchini Bibi Mandisa Mashologu
huko ofisi kwake Chukwani .
Amesema
kutokana na mafunzo hayo hivi sasa
anaridhishwa na utendaji wa wajumbe hao, jambo ambalo limejenga heshima na
imani kubwa kwa wananchi
kuhusiana na Maendeleo ya chombo chao cha Kutunga Sheria.
“
Wajumbe wangu hasa wale wa upande wa
Back Benchers’ (wasiokuwa Mawaziri
/Manaibu Mawaziri) hivi sasa wako
makini, na wanafanya hivyo
kuibana serikali kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji ambapo nguvu hizi wanazipata kutokana na uwezo
wanaojengewa kupitia Ufadhili wa UNDP”
Alisema Spika.
Akitoa
mfano Spiika Kificho amesema Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi tayari wamejengewa
Uwezo katika masuala ya uchambuzi wa
Bajeti na Miswaada ya Sheria na mafanikio yake yameanza kuonekana.
Amesema
kutokana na mafunzo hayo wajumbe wa
Baraza hilo hivi sasa wamekuwa makini
zaidi wakati wa uchambuzi wa Bajeti ya
Serikali na Miswaada ya Sheria kitendo ambacho mara nyengine kinawaweka katika wakati mgumu baadhi ya Mawaziri na watendaji wa serikali
kwa ujumla.
Amesema hali hiyo inapelekea uwajibikaji mzuri wa wajumbe wa Baraza hilo pamoja na Mawaziri suala ambalo ni zuri kwa ustawi wa jamii na
maendeleo ya taifa.
Spika
kificho amemueleza Naibu Mkurugenzi huyo wa UNDP kuwa hata katika utendeji wa
Kamati za Baraza hilo, umeimarika ambapo
hivi sasa kamati zimekuwa zikiibua mambo mengi yanayohususiana na udhaifu au mafanikio ya utendaji wa serikati na taasisi zake.
Hivyo
Spika Kificho amelishukuru shirika hilo kwa misaada yake kwa Baraza la
Wawakilishi na Taifa kwa ujumla na
kuahidi kuendelea kuitumia vyema
fursa inayotolewa na shirika hilo.
Kwa
upande wake Bibi Mandisa Mashologu amesema anaridhishwa na matumizi ya
misaada inayotolewa na shirika hilo kwa Baraza la
Wawakilishi nha kuahidi kuendelea kufanyakazi kwa karibu zaidi na Ofisi hiyo.
Amesema
UNDP iko tayari kuendelea kusaidia vyombo vya kutunga sheria lengo likiwa ni kuimarisha kuongeza uwazi wa utendaji wa taasisis hizo.
Amesema
ni muhimu kwa wananchi kufahamu kwa uwazi
kinachotendeka ndani ya vyombo
hivyo ikiwa ni njia moja wapo ya kukuza
demokrasia na utawala bora hapa nchini.
Kificho huna hataaibu kwamda wa miaka yamapinduzi mnasaidiwa vitendeakazi vya barazani?
ReplyDelete