Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasalimia watoto wa skuli ya Maandali ya Wazazi Amani baada ya kuzinduwa madarasa mapya ya skuli hiyo ya Wazazi,Amani akiwa katika ziara ya kutembelea matawi ya CCM kuimarisha chama ngazi ya matawi hadi taifa.
MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Amani Unguja Ali Mzee Ali, akizungumza katika mkutano wa ziara ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, alipofika katika tawi la CCM Amani kuweka jiwe la msingi la Skuli ya Maandalizi ya Wazazi Amani
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Cheti cha kumaliza mafunzo ya Itikadi ya Chama cha Mapinduzi Masika Kitwana Mustafa, baada ya kumaliza mafunzo hayo yaliowashirikisha Vijana Ishirini wa Wilaya ya Amani. Makabidhisa no hayo yamefanyika katika viwanja vya CCM tawi la Mpendae
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Cheti cha kumaliza Mafunzo kwa Vijana ya Kazi NjeNje, Mwatum Simai, baada ya kumaliza mafunzo yao kwa Vijana wa Wilaya ya Amani,wakati Makamu Mwenyekiti akiwa katika ziara yake kutembelea matawi ya CCM kuimarisha Chama cha Mapinduzi. Katika viwanja vya Tawi la CCM Mpendae Juu
No comments:
Post a Comment