Na
Mwandishi Maalum
Kwa
mara nyingine Bendera ya Tanzania imeendelea kupepea katika Tasnia ya
Ulinzi wa Amani ya Kimataifa.
Mapema wiki hii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon
na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Bi. Nkosizana Dlamin Zuma wametangaza uteuzi
wa Luteni General Paul Ignace Mella
Kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) kuwa Mkuu Mpya wa Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa huko
Darfur ( UNAMID)
Taarifa
iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon, na nakala yake kutumwa katika Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania katika Umoja wa Mataifa,
imeeleza kwamba, Lt. Gen. Mella
anachukua nafasi iliyoachwa na Mkuu
wa zamani wa Jeshi hilo (UNAMID), Lt. Gen Patrick Nyamvumba
kutoka Rwanda ambaye amemaliza muda wake wa
utumishi March 31,2013.
Wasifu
wa Luteni General Paul Ignace Mella unaelezwa
kuwa ni Mwanajeshi wa muda mrefu
na mwenye uzoefu na utumishi uliotukuka
katika JWTZ akiwa amewahi kushika nyadhifa
mbali mbali muhimu za uongozi.
Baadhi
ya nyadhifa hizo ni pamoja na Naibu
Kamanda Kikosi cha Tanzania chini ya Umoja wa Mataifa huko Liberia ( 1993-95), Kamanda wa Kikosi cha JWTZ, Afisa Mnadhimu-Makao Makuu ya Jeshi, Mwambata Jeshi-Ubalozi wa Tanzania
Uganda na hadi sasa alikuwa ni Mkuu wa
Usalama na Utambuzi- JWTZ.
Uteuzi wa Lt. Generali Mella unafuatia
mchakato mrefu ulioshindanisha wateuliwa kutoka nchi mbalimbali duniani, na
hatimaye yeyé akaibuka mshindi.
No comments:
Post a Comment