Habari za Punde

Hadithi ya leo (6)


Mtume Muhammad Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam amesema:

:" إن في الجنة غرفة ..يرى ظاهرها من باطنها ، وباطنها من ظاهرها ..أعدها الله لمن أطعم الطعام ، وألان الكلام   ، وتابع الصيام  ، وصلى والناس نيام " رواه أحمد وحسنه الألباني

Hakika  peponi kuna vyumba, aliyeko nje humuona aliye ndani na aliye ndani humuona aliye nje (transparent). Allaah  ( Subhaanahu Wata’ala) Ameviandaa kwa wenye kulisha watu chakula, wenye kusema kwa maneno mazuri na laini, wenye kuzifuatanisha funga na wenye kusali ( usiku)  ilhali watu ( wengine ) wamelala

Imepokewa na Ahmad na Sheikh Albaani amesema ni hadithi Hasan (nzuri)

Tunapolisha na kuwakirimu waliofunga bila ya kufanya israafu wala kujionesha na kuwalisha wale wanaoihitajia ( maskini na wasiojiweza na mayatima), tunapozungumza na watu kwa maneno ya upole yaliyojaa hekima na busara ndani yake, tunapofunga kwa kuziendeleza bila ya kuzikata kata au kuziacha mkono na tunapoamua kuamka usiku mkubwa kwa ajili ya kusali tu na si vyenginevyo , haya ndiyo malipo ( jazaa) aliyotuandalia Allaah Subhaanahu Wata’ala.

Tumuombe Allaah Subhaanahu Wata’ala atuandalie vyumba hivyi kwa funga zetu tanozoendelea kuzifunga na kwa ibada zetu za usiku tunazoendelea kuzitekeleza.

Aamiyn

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.