Habari za Punde

Buriani Balozi Abraham Isaac Sepetu


Mwanasiasa Mkongwe na Maarufu Zanzibar Balozi  Isaac Abraham Sepetu  amefariki dunia mjini Dar-es- Salaam juzi  kwa ungonjwa wa Kiharusi.

Kwa taarifa iliopatikana kwa ndugu na jamaa  zinaeleza kuwa marehemu alikuwa akisumbulia na uongonjwa huu kwa muda miezi kadhaa, sasa alikuwa akiungua na kusumbuliwa na maradhi ya kiharusi, pamoja na ungonjwa wa kisukari.

Marehemu Sepetu amefariki  juzi mjini Dar-es-Salaam.

 Balozi Sepetu aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, katika miaka ya 1970, wakati wa utawala wa awamu ya kwanza chini ya Rais Mwalimu Nyerere.Vilevile aliwahi kuwa Balozi waTanzania nchini Urusitangu mwaka 1982 wakati wa utawala wa Mwalim Nyerere.

Balozi Sepetu ameshika nyadhifa mbalimbali za uongozi wa juu katika Serekali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serekali ya Mapinduzi Zanzibar  katika vipindi tafaiti

Marchi 27 mwaka huu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, alimteuwa kuendelea na Uwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Uwekezaji Vitegauchumi Zanzibar (ZIPA) wadhifa ambao amekuwa nao hadi kifo chake .

Taarifa iliopatikana mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu maeneo ya Sinza Mori jijini Dar-es-Salaam.


Kwa mujibu wa taarifa za jamaa  zimeeleza kwamba mipango ya mazishi itafanyika katika Kijiji chao Chuwini Wilaya ya Magharibi Unguja siku ya jamatano na mwili wa marehemu utawasili Zanzibar siku hiyohiyo na kuangwa katika kanisa la Minara miwili shangani.saa nne asubuhi.   

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.