Habari za Punde

Basi la Hood laua, lajeruhi

Na Kija Elias, MWANGA
MTU mmoja amefariki dunia huku wengine 16, wakijeruhiwa vibaya, baada ya basi la  kampuni ya Hood  lenye namba za usajili T.488 AXV aiana ya Scania kupata ajali mbaya,  majira ya saa 3:00 asubuhi katika barabara ya Same- Mwanga, wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boaz, ajali hiyo imesababishwa na kupasuka tairi ya mbele na hivyo kusababisha basi hilo kukosa mwelekeo na kuanguka.

Alisema katika ajali hiyo aliyefariki ametambulika kwa  jina la Joshua Likumbia (45),raia wa Kenya, ambaye alikuwa akisafiri kuelekea jijini Mbeya.

Alisema kati ya majeruhi 16, yupo pia dereva wa basi hilo, Fadhili Hashim, ambae amelazwa hospitali ya wilaya ya Same, huku wengene wakitibiwa hospitali ya rufaa (KCMC) ambapo wanane kati yao hali zao sio nzuri.


Aliwataka madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani ili kuepuka ajali zisizo za lazima.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.