Na
Fatuma Kitima, DAR ES SALAAM
RAIS
mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Ali Hassan Mwinyi,amewaasa waislamu kuzitambua fursa
zilizopo na kuzitumia kwa umakini ili waweze kunufaika nazo hasa suala zima la
kiuchumi.
Hayo
aliyasema jana jijini Dar es Salaam
wakati wa ufunguzi wa kongamano la Mashekh na Wanazuoni linalojadili mfumo wa uchumi
wa kiislamu kwa mujibu wa Qur-an na
Sunnah za Mtume (S.A.W) na changamoto
zake.
Amewashauri
Waislamu na wasiokuwa waislamu kujiunga na Saccos, Vicoba, pamoaj na vikundi
vingine vya kiuchumi,kuangalia namana ya kukuza uchumi wao na wananchi kwa
ujumla.
Alisema
kujifunza uchumi wa kimagharibi ambao unapanda na kushuka,hivyo bila
kuelimishana na kuwa na uelewa itakuwa vigumu watu kufahamu mfumo wa kiuchumi
kwa misingi ya kiislamu.
Naye
Mwenyekiti wa kongamano hilo,Shekh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum, ametoa wito kwa walimu wanaofundisha
watoto madrasa, kutoa elimu inayostahili ili kuwajengea vijana uelewa mzuri wa
kutumia fursa zilizopo za kiuchumi.
Aliwataka
Waislamu na wasiokuwa waislamu kutumia fursa za kibenki za kiislamu zinapotokea
kwani benki hizo ni za watu wote na sio jamii fulani pekee.
Kongamano
hilo limeandaliwa na Taasisi ya Walimu wanaofundisha
Qur-an Tanzania (JUWAQUTA).
No comments:
Post a Comment