Na Mwandishi
wetu
MAKAMU
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amekemea tabia ya
baadhi ya watu wanaotorosha kwa magendo
miche ya mikarafuu na kuipeleka nje ya nchi.
Alisema
kitendo hicho hakikubaliki na ni janga kubwa ambalo halina budi kupigwa vita
kwa nguvu zote.
Alisema
hayo jana katika siku ya upandaji miti kitaifa, iliyofanyika katika barabara ya
Cheju-Unguja Ukuu mkoa wa kusini Unguja.
Aidha
alisema serikali itaendelea kuwapa motisha wakulima wa mikarafuu ili kuinua
uchumi na maisha yao
na kuinua pato la taifa kwa jumla.
Ili
kuhakikisha zao la mikarafuu linaimarika, alisema serikali inaendelea kutoa
miche bure na vivutio vyengine, ili kuhakikisha wakulima wanafaidika na jasho
la kazi yao .
Aliwataka
wananchi kupanda mikarafuu pamoja na mazao mengine yakiwemo ya viungo na
matunda kwa sababu haiba na mandhari
njema ya Zanzibar
yataendeela kuwa mazuri iwapo upatikanaji wa matunda mbali mbali na viungo
utaendelea kushamiri.
Alisema
uzinduzi uliofanywa katika katika
barabara ya Jendele hadi Unguja Ukuu ni muendelezo wa kampeni ya upandaji miti
katika barabra na maeneo mengine ya jamii.
Lengo
alisema ni kuhakikisha miti inapandwa katika barabara zote za Unguja na Pemba
na kuhakikisha barabara zinakuwa katika
mandhari nzuri kama ilivyo katika baadhi ya maeneo kama
vile Bungi.
Alitoa
wito kwa skuli na vyuo kupanfiwa program maalum ya kupanda na kutunza miti kwa
wingi.
Aliwaasa
wananchi kuacha tabia ya kukata miti katika viwanja wanavyokusudiwa kujengwa
nyumba zao badala yake wahakikishe nyumba wanazojenga zinazungukwa na miti kwa
kuihifadhi iliyopo na kupanda mingine.
“Wakati
mzuri wa kupanda miti ili istawi na kukua ni nyakati za misimu ya mvua, hivyo
tuzitumie mvua hizi kupanda miti kwa wingi kama itakavyo wezekana,” alisema.
Alisema
serikali kwa kushirikiana na jamii pamoja na vikundi vya kuhifadhi mazingira
imedhamiria kupanda miti katika maeneo mbali mbali ikiwemo hayo ya barabara.
Alisema
jumla ya kilomita 50 za barabara tayari zimepandwa miti katika Wilaya zote za
Unguja na Pemba .
Alisema
ulimwengu umehamanika kutokana na matatizo makubwa yanayosababishwa na
mabadiliko ya hali ya hewa hivyo uhifadhi wa mazingira ni sehemu ya suluhisho
la kupunguza athari za uchafuzi wa mazingira ambazo zinasababisha mabadiliko ya
hali ya hewa yasiyotarajia.
Alisema
juhudi kubwa hazina budi kuchukuliwa katika kutoa elimu kwa wananchi juu ya
umuhimu na thamani ya miti kijamii, kiuchumi na kimazingira na kuonya kwamba
majanga mengi ya kimazingira yataendelea kutokea ikiwa jamii itaendelea kukata
miti hiyo ovyo na bila ya utaratibu.
Mbona Mh. Mizengo Pinda na Viongozi wengine wa Serikali ya Mapinduzi Tanganyika wamekua na mashamba ya Mikarafuu na karibu itazaa... ? Hivo nyinyi Wazanzibari mulikua wapi miaka yote hio hawa wanaokuja kujitia ni Wanyamwezi wakulimia watu mikarafuu wengi wao ni Wizi, usalama, au Majambazi..
ReplyDelete