Na
Masanja Mabula,Pemba
ZOEZI
la uwandikishaji wa vitambulisho vya taifa, limeanza kwa mafaniko katika wilaya
ya Wete kwa shehia za mjini ambapo wananchi waliojitokeza wamepongeza utaratibu
uliowekwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya
Taifa (NIDA).
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi baadhi ya
wananchi, walisema utaratibu uliowekwa na NIDA umeasaidia kuondoa usumbufu na
msongamano wakati wa kuandikisha.
Walisema
utaratibu huo ni tofauti na ule wa uwandikishaji wa vitambulisho vya Mzanzibari
Mkaazi ambapo wananchi wengi hata kama hawana
sifa waliandikishwa.
“
Hakuna budi tuipongeze NIDA kwa kuweka utaratibu na mazingira mazuri ambayo
yatasaidia kuandikisha na kuondoa usumbufu wa kuweka msongamano wakati wa zoezi
hili, ”alisema mmoja wa wananchi.
Naye Mwenyekiti wa masheha wilaya ya Wete ambaye
pia ni sheha wa shehia ya mjini Ole,
Khamis Shaaban Hamad, aliwataka wananchi wenye sifa za kuandikisha wafike
vituoni kama utaratibu uliowekwa na masheha wa
shehia zao.
Alisema
kila shehia imejipangia utaratibu wake ambapo wananchi watakuwa wanaenda kwa
mujibu wa vijiji na kwamba utaratibu huo utawafanya wananchi wote kupata haki yao bila ya usumbufu.
Aidha
sheha wa shehia ya Mtambwe Kusini, Othman Ali Khamis, aliwataka wananchi wenye
sifa kufika kwenye vituo vya kuandikisha wakiwa na vitambulisho vyote
vinavyotakiwa.
Zoezi
la uwandikishaji wa vitambulisho vya taifa limeanza katika wilaya ya Wete baada ya
kumalizika katika wilaya ya Chake Chake na limeanza katika shehia za mjini.
No comments:
Post a Comment