MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba, Juma Kassim
Tindwa, amesema mikoa ya Pemba ni sehemu ya mikoa ya Tanzania, iliyofanya vizuri katika mradi wa TASAF
awamu ya pili na kubahatiaka kuendelea na miradi mengine inayofadhiliwa na TASAF.
Aliyaeleza hayo wakati akifungua mafunzo
ya siku 10 kwa wawezeshaji kuhusiana na
kaya masikini kisiwani Pemba katika ukumbi wa Tassaf Chake Chake.
Aliwataka wawezeshaji hao kuendelea
kuipatia sifa kubwa Pemba katika kutoa kwao
taaluma na kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo.
Alisema wananchi wana matumaini kwamba TASAF awamu ya
tatu itatoa matunda bora zaidi yatakayosaidia kupunguza kasi ya umaskini.
Alisema mpango huo wa kunusuru kaya
masikini zipatazo milioni 1.2 zilizo katika mazingira magumu na hatarishi
kwenye vijiji, shehia na mitaa, unalenga kuhakikisha wananchi wanaishi katika
mazingira mazuri.
Kwa upande wake, Meneja Msajili ya
Walengwa, Phillipien Mmari, alisema awamu ya tatu ya amradi huo utakamilika
mwaka 2012.

No comments:
Post a Comment