Na Himid Choko, BLW
MAKAMO wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa
Balozi Seif Ali Idd amekemea
vikali tabia mbaya ya utoro iliyojengeka kwa baadhi ya wajummbe wa Baraza la
Wawakilishi kutohudhuria vikao vya Baraza hilo.
Mheshimiwa Makamo wa Pili wa Rais ametoa onyo hilo leo
wakati akifunga Mkutano wa 16 wa Baraza la Nane la Wawakilishi ambao pamoja na
mambo mengine ulijadili Bajeti ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa
mwaka wa fedha 2014/2015.
Balozi
Seif amesema si vyema kwa Mheshimiwa
Mjumbe wa Baraza La Wawakilishi kukwepa majukumu yake ya Msingi kwa kukimbia
vikao vya baraza hilo isipokua kwa sababu za msingi zinazokubalika kwa mujibu
wa kanuni za Baraza hilo.
Amesema
kitendo cha Mheshimiwa Spika au Mjumbe yeyote anayeongoza Kikao hicho
kuakhirisha Vikao vya baraza Mara kwa mara kutokana na sababu ya mahudhurio yasiyoridhisha ni jambo
lisilokubalika kidemokrasia , kiuchumi, na kisiasa .
Amesema tabia hiyo ya utoro kwa wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi inakidhalilisha chombo hicho
kikubwa mbele ya macho, masikio na
midomo ya wananchi wanaowawakilishi
majimboni mwao na taifa kwa ujumla .
Amesema
pia kitendo hicho cha Utoro p
kinawanyima haki wananchi kusikia na kuona mambo yao yanazungumzwa na
kutafutiwa ufumbuzi unaofaa.
Aidha
Makao wa Rais amelishauri Baraza la Wawakilishi kubadilisha mfumo wa utoaji wa
posho za vikao vya baraza hilo ili kuweza kuwabana wawakilishi wenye tabia
mbaya ya utoro.
Kwa
mujibu wa wa Kanuni ya 74(2) ya Kanuni za Baraza la Wawakilishi Toleo la 2012 ,
Mjumbe yeyote ambaye bila ya Dharura inayokubalika na Spika au Mwenyekiti wa
Kamati atashindwa kushiriki katika Kikao
cha Baraza na Kamati zake hatolipwa
posho kwa ajili ya kikao hicho na endapo
posho kwa ajili ya kikao hicho imelipwa
mapema , atakatwa kutoka kwenye stahili zake nyengine zitakazolipwa baadae.
Katika
Mkutano huu wa 16 wa Baraza la Nane la Wawakilishi ulioanza tarehe 15 Mei, 2014 , jumla ya maswali ya msingi 66 na 183 ya nyongeza yaliulizwa na waheshimiwa
wajumbe na kujibiwa na Mawaziri wa Sekta
mbali mbali.
Aidha
Mkutano huo ulijadili Hotuba juu ya
Mwelekeo wa hali ya Uchumi na Mpango wa Maendeleo Zanzibar 2014/2015 na
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka
2014/2015.
Mambo
mengine yaliyojadiliwa katika Mkutano huo ni pamoja na Hotuba za Bajeti za Wizara zote 16 za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar na Miswada miwili ya Sheria (Mswada
wa Sheria ya Kutoza Kodi na Kubadilisha Baadhi ya Sheria za Fedha
na Kodi Kuhusiana na Ukusanyaji
na Udhibiti wa Mapato ya Serikali na
Mambao Mengine Yanayohusiana na Hayo pamoja na Mswada wa Sheria ya
Matumizi ya Fedha.
Aidha
Mkutano huo pia ulipokea Taarifa ya Utekelezaji wa Haki za Mtoto kwa mwaka wa
2014/2015 ambapo Miswada miwili ya Sheria
ilisomwa kwa mara ya Kwanza na inatarajiwa kujadiliwa Barazani hapo
katika Mkutano ujao.
Miswada
hiyo ni pamoja na Mswada wa Sheria ya Maadili ya Viongozi Wa Umma na Kuanzisha
Tume ya Maadili ya Viongozi na Mambo Yanayohusiana na Hayo, na Mswada wa Sheria
ya Kufuta Sheria ya Wauguzi na Wakunga
Namba 9 ya Mwaka 1986 na Kuanzisha badala yake Sheria Mpya ya Wauguzi na Wakunga
na Mambo yanayohusiana na Hayo.
Kikao
cha Baraza la Wawakilishi kimeakhirishwa hadi
Siku ya Jumatano ya tarehe 22 Oktoba , 2014 saa 3:00 asubuhi .
No comments:
Post a Comment