Habari za Punde

Balozi Seif afutarisha mkoa wa Kusini Unguja

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akijumuika na wananachi wa Mkoa wa Kusini Unguja katika futari ya pamoja hapo katika Ofisi ya Idara ya Uhamiaji Tunguu Wilayha ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Kulia ya Balozi Seif ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dr. Idriss Muslim Hija na Mkuu wa Wilaya ya Kati Nd. Vuai Mwinyi wakati upande wa kushto yake ni Mkuu wa Wilaya ya Kusini Nd. Haji Makungu Mgongo.
 Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Kusini UInguja wakifutari  pamoja na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisi za Uhamiaji Tunguu.
 Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Kusini UInguja wakifutari  pamoja na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisi za Uhamiaji Tunguu.
 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dr. Idriss Muslim Hija akiwashukuru wananchi wa Mkoa huo waliohudhuria futari ya pamoja kwa niaba ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.

Kushoto ya Dr. Idriss ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif wakati upande wake wa kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kati Nd. Vuai Mwinyi.
 Diwani wa Wadi ya Koani Wilaya ya Kati Nd.Shaaban Jabu Kitwana akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja kwa kumpongeza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kuwaandalia futari ya pamoja.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiagana na Wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja mara baada ya kufutari nao pamoja hapo Ofisi za Ohamiaji Tunguu.

Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.