Na Joseph Ngilisho,
Arusha
JAMBAZI sugu anayetumia
ushirikiana katika kufanikisha matukio ya uhalifu mkoani hapa, ameuawa kwa
kuteketezwa kwa moto na wananchi wenye hasira kali huku hirizi tatu alizokuwa
amejifunga kiunoni zikigoma kuungua.
Jambazi huyo
alitambulika kwa jina la Devii mkazi wa Olisiva mjini Arusha.
Aliuawa baada ya kuvamia
nyumba ya mkazi mmoja akipitia katika tundu dogo la dirisha.
Kwa mujibu wa shuhuda wa
tukio hilo,Emanuel Mejooli ambaye alivamiwa nyumbani kwake na jambazi huyo
,tukio hilo limetokea saa 8.30 usiku wa kuamkia jana wakati akiwa amelala na familia yake.
Alisema alisikia
kishindo kikubwa na baada ya kutoka chumbani alimkuta jambazi huyo akiwa katika
chumba cha watoto.
Alisema baada ya
kumkatama na kumuhoji alijitetea kuwa aliingia ndani kwa lengo la kumfanyia ‘surprise’
halia ambayo ilimlazimu kuita watu na kuanza kumshambulia na baadae walimmwagia
mafuta ya petroli na kumteketeza kwa moto.
Jambazi huyo amekuwa
akijihusisha na matukio ya uhalifu katika maeneo mbalimbali mkoani hapa.
Sapraaaaaiz!!!
ReplyDelete