STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 30.9.2014
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha Wakuu wa Wilaya
pamoja na Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma.
Wakuu wa Wilaya walioapishwa na Dk. Shein ni Bwana Jabu Khamis Mbwana ambaye
ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Micheweni ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa
Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Pemba.
Wengine ni Bwana Amran Masoud Amran ambaye ameapishwa kuwa Mkuu wa Wialaya
ya Wete Pemba, Bwana Hemed Suleiman Abdalla ambaye ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkoani,
Pemba, pamoja na Bibi SSP Sida Mohamed Himid, aliyeapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya
ya Kaskazini “A” Unguja.
Aidha, Dk. Shein amemuapisha Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamisheni ya Utumishi
wa Umma kuendelea na nyadhifa zao kwa kipindi chengine cha miaka mitatu ambapo
Bwana Mohammed Fakih Mohammed ameapishwa kuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya
Utumishi wa Umma.
Wengine ambao wameapishwa kuwa
Wajumbe wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma ni Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Hamid Mahmoud Hamid, Bwana Ali Rajab Juma,
Balozi Hussein Said Khatib, Bwana Issa Mohammed Suleiman pamoja na Bwana
Mabrouk Jabu Makame.
Hafla hiyo, ilifanyika Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi
mbali mbali akiwemo Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi
Khamis, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib Naibu Mufti
Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh
Hassan Othman Ngwali,Washauri wa Rais wa Zanzibar, Wakuu wa Vikosi Maalum vya
SMZ na viongozi wengine wa Serikali
Uteuzi wa viongozi hao umeanza jana tarehe 29 Septemba 2014.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment