Na Miza Othman- Maelezo Zanzibar 14/01/2015
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Ali Juma Shamuhuna amewashauri wahitimu wa vyuo vikuu nchini kutumia elimu na ujuzi wanaopata kujiajiri wenyewe badala ya kusubiri ajira Serikalini.
Hayo aliyasema Chuo Kikuu cha Abdurrahaman Al-Sumaait Memorial Chukwani (Sumait University) wakati wa kuwatunuku shahada ya uwalimu wanafunzi waliohitimu mafunzo hayo katika mahafali ya 14 ya chuo hicho.
Amesema kumekuwa na upungufu mkumbwa wa ajira Serikalini, huku wahitimu wakiendelea kuongeza kila mwaka. hivyo amewataka kutumia taaluma yao kujiajiri wenyewe na kuisaidia jami zao.
“Nnawakumbusha kwamba kuna baadhi ya taaluma soko lake la ajira limepungua, hivyo msikae kusubiri ajira Serikalini bali itumieni elimu na ujuzi wenu ili kujitengezea ajira”, Alisisitiza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali..
Waziri Shamhuna ameupongeza uongozi wa chuo hicho kwa kukipanua na kukipa hadhi zaidi kutoka Chuo cha Elimu na sasa kuwa chuo Kikuu kamili na kupewa jina jipya la Sumait University.
Alisema anaamini kazi hiyo haikuwa rahisi kwa uongozi na wafanyakazi kuitekeleza bali ni matokeo ya kazi ngumu na ushirikiano uliokuwepo kwa kipindi cha miaka mitatu ya mageuzi hayo.
Katika kukiimarisha Chuo Kikuu cha Sumait Waziri Shamhuna ameshauri kuongezwa fani za utafiti na masuala ya ushauri ili kukipa hadhi zaidi na kutoa wanafunzi waliobora.
Aidha aliutaka uongozi wa Chuo hicho kutafuta njia mbadala za kukiendesha badala ya kutegemea zaidi malipo ya wanafunzi na misaada ya wahisani.
Akimkaribisha mgeni rasmi kutunuku shahada kwa wahitimu, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la chuo Dkt. Abdulrahman Al-Muhailan alimpongeza Kaimu Makamu Mkuu wa chuo hicho Professa Hamad Rashid Hikmany na wasaidizi wake kwa kazi kubwa waliofanya katika kukifanyia mageuzi chuo hicho..
Aliishukuru Serikali ya Muungano wa Tanzania kupitia Kamisheni ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kwa ushauri na maelekezo mazuri waliowapa na hatimae kupata usajili katika Kamisheni hiyo.
Alisema sera za chuo hicho katika kipibndi cha miaka mitano inayomalizika mwaka 2017 ni kuwekeza miradi ambayo itaingiza mapato na tayari wameanzisha jingo la ofisi itakayokuwa na ehemu ya kutoa huduma kwa wageni mjini Dar es salaam.
Ameongeza kuwa hivi sasa wanaimarisha Idara ya Uchapaji ya chuo hicho na kuiendesha kibiashara ili kuwavutia wateja kutoka taasisi za umma na binafsi.
Jumla ya wahitimu 266 walikabidhiwa shahda zao katika mahafali hiyo na kufikisha idadi ya wahitimu 1704 tokea kuanzishwa mwaka 1998.
No comments:
Post a Comment