Habari za Punde

Sheikh Soraga ahimiza upendo

Na Mwanajuma Mmanga
Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Fadhil Soraga, amewataka maimamu, walimu wa madrasa na viongozi wa dini, kutumia fursa wanazozipata kuhubiri upendo, mshikamano na utulivu hasa katika kipindi hiki cha kuadhimisha kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW).

Alisema Mtume SAW alikuwa muhubiri mkubwa wa amani na utulivu katika jamii.
Wito huo aliutoa jana wakati akizungumza ofisini kwake Mazizini nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Pia aliwasihi wanasiasa  na kujiepusha na vitendo vyote vinavyosababisha uvunjifu wa amani hasa katika kipindi cha uchaguzi na kura ya maoni kuhusu katiba inayopendekezwa.

Alisema neema za amani na utulivu ni lazima zilindwe na ni wajibu wa kila mmoja kuzienzi na kuzitunza ili zisipotee.

Aidha aliwanasihi Waislamu kuzitumia vyema neema anazopewa na Mwenyezi Mungu.  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.