Na Abdi
Suleiman, Pemba
Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana,
Wanawake na Watoto, Mhe. Zainab Mohammed Omar, amewataka wanachama wa Jumuiya
ya UVIMAWE wilaya ya Wete, kuendelea kukemea na kuelimisha jamii juu ya athari
za vitendo vya udhalilishaji na ubakaji wa watoto.
Alisema hayo baada ya kuuzinduwa Umoja wa Vijana
na Maendeleo wilaya ya Wete (UVIMAWE), katika hafa iliyofanyika Kipangani
wilaya ya Wete.
Aliwataka wanawake watokubali vitendo vya
udhalilishaji na kupiga vita kwa nguvu zote.
Aidha aliwataka wananchi wa Wete kushirikiana
katika malezi ya watoto wao, ili kuweza kuwaepusha na vitendo viovu.
Waziri huyo aliwahimiza vijana kujituma ili
kuweza kuondokana na utegemezi wa ajira kutoka serikalini.
Ofisa Mdhamini wa wizara hiyo, Mauwa Makame
Rajab, alisema wizara yake iko bega kwa bega na UVIMAWE,na kuwasifia vijana wa
Wete jinsi walivyochangamkia fursa mbali mbali zinazojitokeza.
Naye Mwenyekiti wa UVIMAWE, Rashid Shamata, aliiomba
serikali na viongozi kuwasaidia kwa hali na mali ili umoja huo uweze kufikia
malengo iliyojiwekea.
Katibu wa UVIMAWE, Maalim Mohamed Saidi,
aliwashukuru vijana wenzake wa Wete, kwa juhudi yao ya kuanzisha umoja huo utakaosaidia
kupunguza changamoto zinazowakabili.
No comments:
Post a Comment