Habari za Punde

Dk Shein Asisitiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya Kutoa Taarifa kwa Wananchi kupitia Vyombo vya Habari.

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                                                                              16.2.2015
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein amendelea kusisitiza haja kwa  Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutoa taarifa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari ili wajue mambo yanayofanywa katika Mikoa na Wilaya zao.

Dk. Shein aliyasema hayo leo huko Ikulu mjini Zanzibar katika mkutano kati yake na Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ, ulio kuwa na lengo la kuangalia Utekelezaji wa Malengo ya Wizara hiyo kwa robo mbili  kati ya Julai hadi Disemba 2014.

Dk. Shein alisema kuwa huo ni utaratibu uliowekwa na Serrikali hivyo viongozi hao wanatakiwa kutoa taarifa kwa wakati uliopangwa ili wananchi wajue mambo yaliyofanywa na Mikoa, Wilaya zao sambamba na kujua juhudi za maendeleo zinazochukuliwa na   Serikali katika maeneo hayo.

Aidha, Dk. Shein alitumia fursa hiyo, kuwaeleza Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Makatibu Tawala pamoja na viongozi wote husika kuwa tayari Sheria muhimu zimeanza kufanya kazi na kwa upande wao wanakila sababu ya kuzisoma na kuzifahamu kwa lengo la kuwasaidia katika utendaji wao wa kazi ikiwemo Sheria ya Kuongoza Tawala za Mikoa na Sheria inayoongoza Serikali za Mitaa.

Dk. Shein alisema kuwa Sheria hizo zote zina lengo moja na ziko chini ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya SMZ. Pia, Dk. Shein alisisitiza haja ya uongozi wa Mkoa na Wilaya kutoa taarifa juu ya suala zima la ulinzi na usalama kwa Ofisi yao.


Pamoja na hayo, Dk. Shein aliusisitiza uongozi wa Mikoa na Wilaya kuwa na malengo katika kutekeleza Kampeni ya miaka miwili ya kupinga udhalilishaji wa wanawake na watoto sambamba na kuweka utaratibu wa kusimamia katika ngazi za Mikoa, Wilaya hadi Shehia kwani hali ikenda vizuri Kampeni hiyo itafanikiwa.

Dk. Shein pia, aliutaka uongozi wa Mikoa na Wilaya kuoa taarifa juu ya hali ya chakula, lishe na hali ya usalama wa chakula hatua ambayo alieleza kuwa itasaidia kujua suala zima la chakula hapa nchini.

Sambamba na hayo, Dk. Shein aliwataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Makatibu Tawala  kutotumia muda mwingi kukaa maofisini na badala yake waende kwa wananchi hatua ambayo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupata habari mbali mbali na kuwasaidia katika utendaji wao wa kazi.

Aidha, Dk. Shein alirejea kauli yake ya kutaka vijana kushajiishwa juu ya suala zima la ajira na kuitaka Mikoa na Wilaya kuwa na mipango ya kuwasaidia vijana huku akiushauri uongozi wa Mikoa na Wilaya kushirikiana na Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto katika kuwasaidia vijana juu ya suala la ajira.

Alisema kuwa uongozi huo kwa mashirikiano ya pamoja kuwaeleza na kuwapa ushauri vijana sambamba na kuwasaidia kuwapa taaluma juu ya suala zima la ajira ambapo pia, tayari Serikali kwa upande wake imeshachukukua juhudi za makusudi kuanzisha Mfuko wa Uwezeshaji ambao umekuwa ukiwasaidia vijana, kuwapa elimu pamoja na mambo mengineyo katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto hiyo.

Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuungana na Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Wawakilishi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee kutoa pongezi kwa Ofisi hiyo  kwa mafanikio makubwa iliyoyapata ikiwa ni pamoja na mpango mzuri wa Utekelezaji wa Mpango Kazi wa Ofisi hiyo.

Mapema akisoma muhtasari wa Utekelezaji wa Majukumu kwa miezi sita ya mwanzo ya mwaka wa fedha  kuanzia Julai hadi Disemba 2014/2015, Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Haji Omar Kheir  alieleza majukumu, muundo na utekelezaji wa Ofisi hiyo kati ya Julai hadi Disemba 2014.

Aidha, Waziri Kheir alitoa shukurani kwa Dk. Shein kutokana na miongozo na maelekezo anayotoa kwa Ofisi hiyo mara kwa mara kwa lengo la kufanikisha utekelezaji wa majukumu yao ambayo yameweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika utekelezaji wa kazi zao.

Aidha, Waziri Kheir alitua fursa hiyo kutangaza rasmin kuwa Sheria tatu muhimu zimeshaanza kufanya kazi rasmin tokea jana ikiwemo Sheria ya Wakala wa JKU, Sheria ya Kuongoza Tawala za Mikoa na Sheria inayoongoza Serikali za Mitaa.


Katika Mkutano huo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Idd alihudhuria.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.