Habari za Punde

Na Faki Mjaka, Mascut Oman 02/02/2015

Maonesho ya Kimataifa ya Sanaa,Ubunifu na Utamaduni yanayoendelea Mascut 

nchini Oman yamechukua sura mpya baada ya Nchi Washiriki kupeleka Wasanii wake wa 

Ngoma za Asili kwenda kutumbwiza katika wiki mbili za mwisho ya Maonesho hayo.


Tanzania ni moja ya nchi washiriki ambapo Wasanii wake 15 Usiku wa jana walipata nafasi 

ya kuburudisha kwenye Jukwaa kuu la Maonesho hayo.


Akizungumza kuhusu ujio wao Kiongozi wa Wasanii hao wa Ngoma Bi Asha Khatib 

amesema wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanazikonga vyema nyoyo za Waomani kwa 

burudani ya nguvu.


Amefafanua kuwa Waoman wengi wanapenda Ngoma zenye asili ya Zanzibar hivyo 

wamefanya Mazoezi ya kutosha ili kuwafurahisha Mashabiki wao pale wanapopanda 

Jukwaani kwa ajili ya kutumbuiza.


“Kwa kweli tumejiandaa vizuri tu na tumekuja hapa Mascut kwa kazi moja tu ya kutoa 

Burudani hivyo Waoman wazidi kuja kwa wingi kuja kujionea burudani ya aina yake yenye 

Asili ya Tanzania-Zanzibar”Alisema Bi Asha.



Bi Asha amebainisha kuwa katika Jukwaa watapiga baadhi ya Ngoma zenye Asili ya 

Zanzibar kama vile Msewe, Uringe, Gonga, Kyaso,Kitua tua,Kibunguu na Kidumbaki 

ambapo anaamini zitakidhi kiu ya burudani kwa Waomani.


Jana ikiwa ni siku ya mwanzo kwa Watanzania hao hivyo walipewa muda wa nusu saa kwa 

ajili ya kusalimia jukwaa na kutumbuiza ambapo walipiga Ngoma ya Msewe na Kitua tua.


Kabla ya Watanzania kupanda Jukwaani kwenda kutumbuiza walitanguliwa na Wasanii 

kutoka Ufaransa ambapo baada ya Watanzania kumaliza Wasanii kutoka Urusi ndio 

waliochukua nafasi kutumbuiza.


Nchi nyingine zilizopata nafasi ya kutumbuiza katika Jukwaa kwenye Maonesho hayo ya 

Kimatifa ya Sanaa, Ubunifu na Utamaduni ni pamoja na China, Iran, Thailand, India, 

Uzbekistani na Misri.


Kwa wiki mbili mfululizo kuanzia jana Wasanii wa Nchi hizo zinazoshoriki Maonesho ya 

Kimataifa ya Sanaa,Ubunifu na Utamaduni watakuwa wakipanda katika Jukwaa kuonesha 

vipaji vyao vya Muziki wa Asili ya nchi zao husika.


Wasanii hao wa Ngoma waliofika Juzi kutoka Tanzania wanaungana na Wenzao 

waliokuwepo Oman kwa zaidi ya wiki mbili sasa kushiriki Maonesho hayo ambapo Wasanii 

huonesha bidhaa zao wanazozitengeneza kwa Mikono na kuwauzia Wateja mbalimbali 

wanaofika katika Maonesho hayo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.