Habari za Punde

Kikao cha kutathmini juu ya utendaji wa kazi za waandishi Pemba

 MWANDISHI wa Habari wa Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar Ofisi ya Pemba, Haji Nassor Mohamed akitoa maelezo kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari, katika kikao cha kutathmini juu ya utendaji wa kazi za waandishi hao, mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Habari Maelezo Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WAANDISHI wa Habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari kisiwani Pemba, wakisikiliza maelezo kutoka kwa mwandishi wa habari mwandamizi kisiwani Pemba, Haji Nassor Mohamed katika kikao cha kutathmini utendaji wa kazi za waandishi huko katika ukumbi wa Habari Maelezo Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MRATIB wa Tume ya Utangazaji Pemba, Afani Othman Juma akitoa nasaha zake kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari, huko katika ukumbi wa Habari Malezo kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MWENYEKITI wa kikao cha waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari Pemba, ambae pia ni mwenyekiti wa Pemba Press Club (PPC) Khatib Juma Mjaja akitoa nasaha zake kwa waandishi wa habari huko katika ukumbi wa Habari Maelezo Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
MKUU wa shirika la magazeti ya Serikali ya Zanzibar Ofisi ya Pemba, Bakar Mussa Juma akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari kisiwani Pemba, huko katika ukumbi wa Habari Maelezo Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.