Mke wa Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete
amefurahishwa na hatuwa iliyochukuliwa na Walimu wa Jimbo la Uzini Zanzibar ya
kufanya ziara ya kimasomo Mkoani Lindi kwani ni njia moja wapo ya kujifunza na kujiongezea
elimu kwa vitendo.
Hayo ameyasema Jana wakati akiwakaribisha walimu wa Jimbo hilo Mkoani hapo kwa ajili ya kuanza rasmi ziara yao ambayo inatarajiwa
kuchukuwa takribani wiki moja.
Aidha Mama Salma amesema ziara za kimasomo ni njia moja ya kuleta
mashirikiano na kudumisha Muungano wa Watanzania katika kuboresha Sekta ya
Elimu Nchini hiyo ni kwa sababu Elimu ya
Juu na Sekondari nchini Tanzania
ni moja ya mambo yaliyo chini ya Serikali ya Muungano.
Akizungumzia Changamoto zinazowakabili Walimu hao katika Sekta ya Elimu kwa upande wa Mkoa wa Lindi ni upungufu wa
walimu wa masomo ya Sayansi jambo ambalo husababisha kukosekana kwa wataalamu wa fani
mbalimbali za Kisayansi kwa maendeleo ya Taifa ambapo hurudisha nyuma jitihada zao za kutaka
kuzalisha wataalamu watakaokwenda sambamba na ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia.
Nae Afisa Uendeshaji wa Wizara ya Elimu Zanzibar Nd. Muhussin Sufiani
Mkanga amesema lengo kuu la ziara hiyo ni kujifunza njia mbalimbali zilizobora
za kielimu ikiwa ni njia za kuwafundishia wanafuzi wa Zanzibar katika kuimarisha ufaulu mzuri kwa
wanafunzi wa Kidato cha Nne.
Hata hivyo amewataka walimu wenzake waliopata fursa kuwepo katika ziara
hiyo kuwa makini katika kujifunza masomo hayo kwa lengo la kupata njia zilizo
bora za utoaji wa elimu kwa wanafunzi wao ikiwa ni mfano mzuri wa kuigwa
na walimu wengine Nchini.
Jumla ya walimu 36 kutoa Zanzibar wamepata
fursa ya ziara ya kimasomo Mkoani Lindi na wanatarajiwa kuwa mabalozi wazuri
kwa walimu wenzao waliokosa fursa hiyo kwa kuwapa yale yote mazuri waliyoyapata
na kuyafanyia kazi kwa maendeleo ya Nchi yao .
IMEHARIRIWA NA HABARI
MAELEZO-ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment