Habari za Punde

Aliyeiba jembe afungwa miezi miwili

Na Hassan Khamis, Pemba

MAHAKAMA ya mwanzo Wete, imetoa hukumu ya kifungo cha miezi miwili kutumikia chuo cha Mafunzo, kwa mshtakiwa Luhasa Ndengule Kashere (20) mkaazi wa Junguni Gando, aliyedaiwa kuiba jembe moja.

Mara baada mshtakiwa kupanda kizimbani akisubiri taratibu za mahakama, ndipo hakimu wa mahakama hiyo Abubakar Suleiman Thabit alipotoa hukumu hiyo kwa mshatikiwa.

“Mshtaliwa, kwa vile ni kosa lako la mwanzo na hatuna kumbukumbu ya makosa uliyofanya nyuma, adhabu yako kutokana na kosa hili ni miezi mitatu lakini nakufanyia tahfifu, utatumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miezi miwili”, alisema Hakimu huyo.

Hakimu huyo amesema kilimo ni uti wa mgongo wa taifa hivyo kitendo cha kuiba jembe ni sawa na kuvunja uti huo wa mgongo hivyo mahakama imejiridhisha na maelezo yalitolewa na mashahidi wa pande zote mbili.

Mwendesha mashtaka wa Polisi stesheni sajenti Khamis Faki Simai alidai mahakani hapo kuwa April 5, mwaka huu baina ya saa 4:00 asubuhi na saa 8:00 mchana, bonde la bibi Wangoji Junguni Gando Wete Mshtakiwa alliba jembe moja la kulimia lenye thamani ya shilingi 6000 mali ya Thani Juma Hamad.


Kufanya hivyo ni kosa kinyume na vifungu 267 (1) na 274 (1) vya kanuni ya adhabu sheria namba 6 ya mwaka 2004, sheria ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.