Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Japan Batilda Burian aliyeteuliwa hivi karibuni na kufika Ikulu Mjini Zanzibar leo
kujitambulisha,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Japan Batilda Burian aliyeteuliwa hivi karibuni na kufika Ikulu Mjini Zanzibar leo kujitambulisha,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi wa Malawi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hawa O.Ndilowe alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo kujitambulisha kwa Rais,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiagana na Balozi wa Malawi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hawa O.Ndilowe baada ya mazungumzo yao leo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha,[Picha na Ikulu.]
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 6.5.2015

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesisistiza haja ya kuimarisha zaidi uhusiano
na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Japan hasa kwa kutambua hatua za nchi
hiyo za kuendelea kuiiunga mkono Tanzania katika kuimarisha miradi mbali mbali
ya maendeleo hapa nchini.
Dk. Shein
aliyasema hayo leo huko Ikulu mjini Zanzibar, wakati alipofanya mazungumzo na
Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Japan Mhe. Batilda
Buriani.
Katika mazungumzo
hayo Dk. Shein alimueleza Balozi huyo Mteule kuwa Tanzania ikiwemo Zanzibar
inajivunia uhusiano na ushirikiano sambamba na hatua za Japan za kuendelea
kuiunga mkono Tanzania katika kuimarisha miradi kadhaa hapa nchini.
Dk. Shein alisema
kuwa kwa upande wa Zanzibar, Japan imekuwa mshirika mkubwa katika kuunga mkono
uimarishaji wa miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kusaidia mradi mkubwa wa
maji ambao hivi sasa upo katika awamu ya pili sambamba na usambazaji wa huduma
za umeme pamoja na miradi mengineyo.
Aidha, Dk. Shein
alisema kuwa mbali na juhudi hizo za nchi ya Japan kwa Tanzania kwa vile
Zanzibar imekuwa ni miongoni mwa visiwa maarufu kiutalii duniani ipo haja ya
kuendelea kuitangaza Zanzibar nchini humo ili wataalii wa Japan waje kuitembea
Zanzibar kwa wingi.
Pamoja na hayo,
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kumueleza Balozi Burian azma ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha sekta ya uvuvi hapa nchini.
Dk. Shein pia,
alimueleza Balozi huyo haja ya kuikuza na kuiimarisha lugha ya Kiswahili kwa
kutambua kuwa hivi sasa lugha hiyo imekuwa na nafasi kubwa duniani ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa redio ya
kiswahili nchini humo.
Kutokana na hatua
hiyo Dk. Shein alisema kuwa ipo haja ya kuikuza lugha hiyo kwa kukitangaza Chuo
Kikuu cha Taifa cha Zanzibar SUZA nchini Japan, ambacho kimekuwa na Kada ya
Kiswahili kinachofundishwa kwa wageni.
Nae Balozi huyo
Mteule wa Tanzania nchini Japan Mhe. Batilda Burian alitoa pongezi kwa Dk.
Shein pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho
Kikwete kwa kupata uteuzi huo mpya ambapo kabla ya uteuzi huo alikuwa Balozi wa
Tanzania nchini Kenya.
Balozi Burian
alimuhakikikishia Dk. Shein kuwa katika wadhifa wake huo mpya juhudi za
makusudi atazichukua katika kuhakikisha uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya
Japan na Tanzania unaimarishwa zaidi.
Wakati huo huo, Dk. Shein alifanya mazungumzo na Balozi wa Malawi
nchini Tanzania Mhe. Hawa Ndilowe na
kumueleza kuwa Zanzibar ina historia kubwa ya uhusiano na ushirikiano kati yake
na Malawi na kusisitiza haja ya kuimarishwa.
Katika mazungumzo
hayo, Dk. Shein limueleza Balozi huyo kuwa hivi sasa Zanzibar kutokana na kukua
kwa sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kuimarika kwa vyuo vikuu hapa nchini
wananchi kutoka Malawi wamekuwa wakipata fursa ya kusoma katika vyuo vikuu vya Zanzibar.
Aidha, Dk. Shein
alimueleza Balozi huyo azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kukuza
sekta zake za maendeleo ikiwemo sekta ya kilimo ambayo alisema ushirikiano wa
kitaalamu unahitajika katika sekta hiyo kwa pande mbili hizo.
Kwa upande wa
sekta ya biashara, Dk. Shein alisema kuwa wafanyabiashara wengi wa Malawi
wamekuwa wakifanya biashara zao nchi Tanzania na kusisitiza haja ya
wafanyabiashara hao kuja Zanzibar kwa ajili ya kufanya biashara ya viungo
ambavyo itakuwa ni kivutio kikubwa kwa watalii kutoka nchini humo.
Mbali na
ushirikiano katika sekta za maendeleo pia, Dk. Shein alieleza kuwa kutokana na
wananchi wa pande mbili hizo kushabihiana kiutamaduni kuna haja ya kushirikiana
katika kukuza sekta hiyo.
Nae Balozi Hawa,
alimpongeza Dk. Shein pamoja na Serikali anayoiongoza kwa mafanikio makubwa
yaliopatikana hapa Zanzibar na kumueleza kuwa Malawi ina mambo mengi ya
kujifunza kutoka kwa ndugu zao wa Zanzibar.
Balozi Hawa
alieleza kuwa Malawi inathamini uhusiano na ushirikiano wa kihistoria kati ya
nchi hiyo na Zanzibar tokea wakati wa Waasisi wa pande mbili hizo na kuahidi kuwa
hatua hiyo itaimarishwa na kuendelezwa.
Pamoja na hayo,
Balozi Hawa alimueleza Dk. Shein kuwa mbali ya azma ya nchi yake ya kuendeleza
uhusiano na ushirikiano katika sekta za maendeleo ikiwemo kilimo, elimu,
biashara, utamaduni na nyenginezo pia, Malawi itapata fursa ya kupanua wigo
kwenye sekta ya utalii ambayo kwa Zanzibar tayari imeshapiga hatua.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment